Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuchangia Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Wananchi miaka ya nyuma ilikuwa inaonesha hali nzuri sana katika hali za michezo. Tunajua michezo inatambulisha Taifa, kwa hiyo, nilikuwa ninaomba Jeshi hili liendelee kuhimiza wanamichezo jeshini waweze kuisaidia Tanzania. Tunakumbuka kina Nyambui waliitambulisha Tanzania vizuri sana nyakati zile, sasa hivi mimi kama promoter wa ngumi tuna wachezaji watatu tu kutoka jeshini. Tuna wanangumi watatu wanatuwakilisha nje ya nchi kutoka jeshini, sasa Jeshi haliwezi kutupa wanangumi watatu, tunaomba muongeze wachezaji wa ngumi maana ngumi inalipa na inatambulisha Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nipende kumtambua Suleiman Gariatano ambaye ni mwanajeshi anatuwakilisha vizuri, Suleiman Kidunda anatuwakilisha vizuri, Bonabuchi anatuwakilisha vizuri, lakini JKT ina msichana Mnyakyusa mwenzangu Grace Mwakimere naye ni mpiga ngumi mzuri sana. Ninaomba tusimamie michezo ya ngumi Jeshini maana itasaidia kuisaidia Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niende kwenye nyumba za wanajeshi. Mimi nimezaliwa kwenye Kambi ya Jeshi nyumba za jeshi kwa mfano quarter zile za Keko mpaka leo zimechaka, ukienda nyumba za Mwenge pale Mwenge magorofa ni chakavu sana. Ninashukuru kwamba mmejenga mwaka 2025 mpaka mwaka 2020 mmejitahidi sana kujenga nyumba, lakini zile za zamani mmeziacha kuzikarabati. Ninaomba bajeti hii muweze kuzikarabati wazazi wetu waweze kuendelea kukaa katika mazingira mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia suala la maduka yale ya bei nafuu yaliyokuwa jeshini, yalikuwepo kwa muda mwingi mpaka sisi tunakua yalikuwepo, lakini miaka sita iliyopita yalisitishwa. Ninaomba yarudishwe kwa sababu wazazi wetu hawa na wanajeshi wetu na makamanda hawa hawana muda wa kufanya biashara zingine. Kwa hiyo, mkiwapa eneo la kwenda kununua vitu bei rahisi mnakuwa mmewasaida na kuwapa motisha. Tusiwaache tu wakaishia kufuga bata na kuku kwenye quarters zetu. Tunaomba warudishiwe yale maduka ili waweze kupata vitu kwa bei rahisi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia suala la upandishwaji vyeo hasa wanawake, ninajua Waziri wewe ni mwanamke, ninaomba utazame wanawake makamanda, ambao bado wako Jeshini wanaofanya kazi vizuri wapandishwe vyeo kwa haraka. Najua hatupandishi cheo kwa sababu ni mwanamke, ninafahamu, kwa sababu, wako jeshini ni makamanda ninajua wana uwezo wa kupandishwa vyeo na wana uwezo wa kufanya kazi yao vizuri.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo suingi hoja, aah naunga hoja. (Makofi/Kicheko)