Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Stergomena Tax (Mb) Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Katibu Mkuu pamoja na Mkuu wa Majeshi kwa niaba ya Jeshi letu lote la Ulinzi na Kujenga Taifa nchini. Kipekee kabisa napenda kumpongeza sana Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiweka nchi yetu kuwa salama, yenye amani na utulivu.

Mheshimiwa Spika napenda pia kuwapongeza kwa ushirikiano wanaotoa kwa mamlaka mbalimbali katika kuleta amani na kuifanya dunia kuwa mahali salama pa kuishi. Nawapongeza pia kwa kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ya kijamii.

Mheshimiwa Spika, ombi letu, kama ambavyo nimekuwa nikichangia katika mipango mikakati yenu ni vema barabara za mpakani ikiwemo Mbamba bay – Lituhi; kufungua barabara ya mpaka wa Tanzania na MsumbiIji ikiambaa na mpaka wetu, kama ambavyo miaka 1970 ililazimu kufungua barabara ya Mbamba bay - Lituhi kufuatia chokochoko za Malawi. Ni vema kujiweka sawa; na kuboresha makazi ya kiteule cha Liuli na gari.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.