Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee nikushukuru sana kwa kunipa hii nafasi, lakini nichukue nafasi hii nimshukuru sana ndugu yangu Mheshimiwa Nape, Waziri na Naibu Waziri kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya. Vilevile niwashukuru sana ndugu zetu wa USCAF, TTCL na timu nzima ya Mheshimiwa Nape ambayo kwa kweli wanafanya kazi kubwa. Hatuna mashaka na Mheshimiwa Nape, tunajua alivyo aggressive, alivyo determined na amedhamiria kubadilisha hii Wizara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nina mambo machache. La kwanza, naomba nijadili kuhusu umuhimu wa hii Wizara. Sasa hivi ukiangalia Tanzania tulipo, Wizara hii ya TEHAMA ndio engine ya maisha yetu ya kila siku, ni engine ya uchumi, ni engine ya mawasiliano, ni engine ya kila kitu. Sasa wakati nafikiria ni jinsi gani nakuja kuchangia kwenye hii Wizara, nilikuwa naangalia hii Wizara nai-position wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia Wizara zote, zinategemea Wizara ya Mheshimiwa Nape. Watu wa fedha wanamtegemea Mheshimiwa Nape, watu wa afya wanamtegemea Mheshimiwa Nape, watu wa kilimo wanamtegemea Mheshimiwa Nape, watu wa maji wanamtegemea Mheshimiwa Nape. Hii ni Wizara ambayo ni pivotal. Ni Wizara ambayo ipo at the center. Mheshimiwa Nape ni refa anayehakikisha kwamba ili utoaji wetu wa huduma unaotolewa kwa njia ya TEHAMA, Wizara ya Maji, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Afya, unafanikiwa lazima tumwezeshe Mheshimiwa Nape. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu kubwa ni nini? Sisi kama nchi tunahitaji kui-brand hii Wizara. Hii ndio Wizara mama, Wizara ambayo imebeba maisha yetu, Wizara ambayo imebeba uchumi wetu. Hapa tunaongea kwa kutumia hii technology ni kwa sababu imewezeshwa na Wizara ya Mheshimiwa Nape. Tunatumia vishikwambi ni kwa sababu ya Wizara ya Mheshimiwa Nape. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wito wangu ni nini kwa Serikali? Kwanza nina mambo mawili; la kwanza, ufike muda sasa tufanye reformation ya hii Wizara. Hii Wizara inatakiwa kukaa kwenye muundo upi? Hii Wizara inatakiwa ikae katikati i-coordinate zile Wizara zote, lakini sidhani kama hiyo structure, hiyo business modal na coordination modal imekuwa well defined. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naishauri Serikali ifikirie upya tunai-position vipi Wizara ya TEHAMA ili kuhakikisha kwamba sasa inajionesha na inatoa ile coordination support vizuri sana katika Wizara nyingine? Hilo lilikuwa la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwanza nichukue nafasi hii nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri. Mwaka 2021 alinitengea fedha kwa ajili ya kujenga minara ya simu kule Mangoli na Heka kwa kupitia TTCL na tayari tumeshajenga ile minara. Mnara wa Mangoli umeshaanza kufanya kazi, mnara wa Hika umeshakamilika na tunasubiri kuuwasha. Bado kuna maeneo yana shida sana ya mitandao. Kuna Kijiji cha Igwamadete, Simbangulu, Mbweko, Magasai, Kapiti na vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii nimshukuru vilevile Mheshimiwa Waziri, katika bajeti hii hivi vijiji vyote ameviingiza kwenye bajeti, nashukuru sana. Wito wangu ni nini? Wengi wameongea hapa, sidhani kama tunahitaji kujenga kila aina ya mnara, Vodacom, TTCL kwenye kila Kijiji. Tunahitaji ku-integrate hizi services. Kwa hiyo, wito wangu kwa Mheshimiwa Nape, kaa na timu yako m-brainstorm, mje na modal ambayo itakuwa very cost effective kuhakikisha kwamba, Voda, Halotel, TTCL, watatumia mnara mmoja, hiyo itatusaidia sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)