Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi kwa ajili ya muda ninaipongeza Serikali pamoja na viongozi wote wa Wizara. Mchango wangu utajielekeza kwenye mapinduzi ya nne ya viwanda Forth Industrial Revolution nikimaanisha nataka kuongelea teknolojia ya Block Chain.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kabla nijielekeze kwenye mchango wangu naomba nitaje baadhi ya maeneo kwenye Jimbo langu ambayo hakuna mawasiliano ya simu. Kata ya Mkomba yote especially kwenye kijiji cha Ntungwa, kijiji cha Mfuto, Isunda, Lwasho, Kata yote ya Kapela na vijiji vyake Lwate, Ntanga, Ntungwa, Mang’ula pamoja na vijiji vingine kata ya Ivuna Kamsamba na Chiluluma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuchangia kwenye block chain nataka kuongelea kwenye hili eneo ambalo angalau Benki Kuu yetu imeshaanza kuruhusu mazungumzo na baadhi ya vijana wa kitanzania ambao wanafanya kazi kwenye hii teknolojia nataka niseme toka teknolojia hii imeingia kwenye mapinduzi haya ya nne ya viwanda zaidi ya vijana wa kitanzania 1,000,000 pamoja kwamba siyo rasmi wanajishughulisha na biashara hii na kwa miaka minne au mitano ambayo imepita zaidi ya bilioni 300 za kitanzania zimeshafanyiwa transaction lakini unaweza ukaona hakuna namna nzuri ambayo Serikali imeweka ili kuendelea ku-regulate hizi transaction ili iweze kuzichukulia kodi lakini pia ili kuilazimisha hii sekta na tuweze tufahamu tupate takwimu kwamba ni watanzania wangapi ambao wanajihusisha na hii teknolojia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hii Central Bank Digital Currency nataka nirejee waraka mmoja ambao umepita kama wiki mbili Benki Kuu walitoa, ambao ulikuwa unasema hivi Ministry and chamber welcomes discussion on CBDC and clip to asset Minister for Finance and Planning Dr. Mwigulu Nchemba has challenge an International Conference on Central Bank Digital Currencies and clip to assets to come up with a clear guidance and whatever countries should regulate or supervise clip to assess or discourage their use.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema kwamba hapa wanasema whether waone namna nzuri ambayo wanaweza waka-regulate au wakaamua kui-discourage nataka kusema ni ngumu sana kama Serikali kupitia Wizara hii ambayo inasimamia suala hili kama hawataruhusu kutengeneza chombo maalum ambacho watawaita vijana wa kitanzania ambao wanauelewa waweze kuwashauri waweze kuwasaidia ndipo ambapo watakuja na njia nzuri ya kuweza kuwasaidia namna ya ku-regulate kuwepo kwa hii Benki ya hii CBDC yaani tupate Central Bank ambayo itajishughulisha na mambo ya digital currencies. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, itakuwa ngumu kwa sababu gani? Kwa sababu hoja ya CBDC huko duniani ni kuwepo kwa beat coin (yaani ni kuwepo kwa zile digital currencies) hoja na idea na concept ambayo iko kwenye block chain ambayo iko kwenye digital currency especially kwenye beat coin ndiyo ambayo huko duniani iliibua hii CBDC. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa itakuwa ngumu sana kui-regulate na kuipokea hii idea ikiwa kama tu kwanza Serikali haijawahi kumiliki hata coin exchanger yoyote hapa tunapoongea sidhani kama Serikali wanajua kuna kitu kinaitwa Binance, kuna kitu kinaitwa Remitano local bitcoin. Tulitamani kuona angalau kuwe hata na coin exchanger yoyote ya majaribio ambayo Serikali imefanya vijana hawa wa kitanzania wana-practice na wana-regulate sasa hatujawahi ku-regulate unafikiri Benki Kuu wataichukulia hii namna gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwenye Wizara hii ninawaomba mtoe room under Task Force yako ita vijana wa kitanzania wakupe ushauri hatupotezi chochote kama tutakubali kujifunza. Naomba nitolee mfano mimi nikiwa form two mwaka 2004 tulikuwa tunafundishwa kama siyo form two form three kuna topic moja ilikuwa inasema globalization. Tulikuwa tunaambiwa dunia kiganjani at that time kulikuwa hakuna smart phone unaposema dunia kiganjani tulikuwa hatujui tutamaanisha nini dunia kiganjani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sasa hivi tuna-practice dunia kiganjani bili tunalipia kwenye kiganja, Bunge tunaendesha kwenye kiganja habari ni kwenye kiganja. Kwa hiyo, hata hili jambo ili CBDC iweze kufanyakazi ni lazima kwanza Serikali iruhusu vijana wa kitanzania ni lazima Serikali iwekeze iweze kuleta coin exchange Serikali ifungue wallet ifanye majaribio kama ambavyo tunaweza tukasema hatuna vita Jeshini lakini tunatengeneza mabomu kwa kujihami tu kwamba likitokea lolote tufanye, kwa hiyo, tungeweza kufanya mazoezi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mzuri Rais wa Salvador ambaye anaitwa Naibu Bukin tarehe 17 Mei Jumanne hii ya wiki hii ambayo tuliyonayo aliitisha mataifa 44 duniani akiziita baadhi ya Benki Kuu kwenye mataifa mbalimbali, lakini akiziita na baadhi ya taasisi za kifedha kwenda kushiriki akaunti yake ya twitter iko verified wataalam wanaweza wakamtembelea wakaona pale unaweza ukatembelea page yake Waziri ukaona alichokifanya na majadiliano yote aliyofanya. Rais huyu aliziita nchi mbalimbali Zambia ilikuwepo, Mauritius ilikuwepo, Bangladesh, Mozambique, Morocco, Sera Leone, Senegal, Nigeria, Jordan, Egypt na nchi mbalimbali kwanini sisi nchi yetu hakutokea hata mwakilishi hata mmoja tunapoteza hela nyingi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tunaendelea kulalamika tunasema kwamba ajira ni ngumu kwa watanzania ni kweli ajira ni ngumu na tukiwa hapa Bungeni tunalalamika kila wakati kwamba mfumo wetu wa elimu hau-support watu kujiajiri, lakini tunashindwa kuendana na teknolojia.

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Condester.

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, dakika moja tunashindwa kuendana na teknolojia tuliyonayo ili iweze kuwaajiri vijana wengi wa kitanzania na kupoteza mapato. Wito wangu kwa Serikali kwenye bajeti hii unda chombo kwenye Wizara yako Mheshimiwa Waziri Nape ili vijana wa kitanzania waweze kukushauri na tuweze kuitumia vizuri Block Chain Technology naunga mkono hoja. (Makofi)