Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi na kuwa mchangiaji wa mwisho nakushukuru sana. Kwanza kabisa nimshukuru sana Mheshimiwa Rais Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu nzima ya Wizara hii. Nimshukuru vile vile Mkurugenzi wa UCSAF kwa kweli kati ya wakinamama wanaofanyakazi vizuri sana Wakurugenzi wenye customer care inayotisha kwa kweli, kwa kweli anatisha sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiteto tulikuwa na changamoto kubwa sana ya mawasiliano watanzania wa Kiteto kwa miaka karibu 60 ya uhuru walikuwa hawawezi kufuatilia Redio Tanzania na mitandao ni tabu sana alikuja Mheshimiwa Naibu Waziri Eng. Kundo tarehe 21 Januari kwa kweli tume-drive kilomita 240 siku moja kuanzia saa mbili ya asubuhi mpaka karibu saa mbili usiku nafarijika sana kwamba kwenye bajeti hii ukurasa wa 145 vijiji 25 Kiteto ipo kwenye mipango ya mwaka wa fedha 2022/2023 nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri nawashukuruni sana kati ya vijiji ambavyo vilikuwa vinasumbuliwa na mtandao Esuguta, Ndotoi, Laiseri, Nsolosidan, Morokitikiti, Engangware, Amey, Lembampuli, Lolera, Emarti, Nati, Magungu, Kinua, Ndirigish, Taigo, Krash, Ndaleta, Orpopog, Mwitikira, Kiperesa, Asamato, Kimana na Songambele na Loltebes zote ziko kwenye bajeti ya Serikali nawashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Redio Tanzania ilikuwa haisikiki kati ya wilaya saba ambazo imepangwa kwamba wataenda ku-revolutionize ili na sisi tupate Redio Tanzania kwa mara ya kwanza Kiteto imo nakushukuru sana Wizara hii kwa kweli tuipitishe hii bajeti kwa haraka sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na suala lingine moja tu dogo Mheshimiwa Waziri kumekuwa na mtandao watu wanatupigia simu wanajifanya ni customer care wa makampuni ya simu anajifanya anakupigia anakutapeli watanzania tumekuwa tuki-volunteer kuripoti hizi namba kwa makampuni hayo hatupati taarifa kwamba ile namba uliyoripoti tumefanya hivi tukifanya hivyo take them to task na sisi tutaendelea kuripoti hizi crimes ili watanzania wasitapeliwe nakushukuru sana ahsanteni sana na Mwenyezi Mungu awabariki sana. (Makofi)