Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaishukuru Serikali imeandaa sera na sheria kwenye sekta za TEHAMA, sayansi na ubunifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili Serikali iweze kuisimamia vizuri sekta ya TEHAMA tunahitaji kwa haraka sana kuanzisha ICT Professional Regulation (ICT Commission haijafanya kazi ya kufanya regulations) imara kama wenzetu kwenye sekta zingine mfano wahasibu, afya, na kadhalika. Tumeona CAG akiibua mambo kibao kuhusu mifumo yetu ya taarifa/TEHAMA tunaweza kuhakikisha maadili na weledi kwenye sekta ya TEHAMA bila kuwa na Bodi ya kuwasimamia waatalamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna mwingiliano mkubwa wa majukumu kati ya baadhi ya taasisi za Serikali mfano TCRA, eGA, COSTECH, ICT Commission na Wizara za Utumishi, Elimu na Mawasiliano. Ni vizuri tukawa na taasisi moja inayosimamia au kupunguza mwingiliano na kutumia vizuri rasilimali

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashukuru Serikali kuanzisha matukio mbalimbali ya kuinua vipaji (innovation weeks) kwa mfano MAKISATU ambapo vijana wameonesha matumizi ya TEHAMA na ubunifu mwingine kusaidia sekta za elimu, afya na kadhalika. Changamoto kubwa ni kuweza kuwa na mfumo mzuri wa kitaasisi na endelevu wa kuwatambua na kuwaendeleza wale wenye products/innovations ambazo zitakuwa na faida kwa vijana hawa na Taifa kwa ujumla. Iko wapi Silicon Valley ya Tanzania? Ahsante.