Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza kwa kazi nzuri lakini zaidi ushirikiano kuanzia Wizarani hadi watu wa Mfuko wa Mawasiliano na TCRA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mafinga tumekuwa wanufaika wa TCRA, wameshatusaidia katika shule ya msingi mchanganyiko ya Makalala yenye watoto wenye mahitaji maalum na pia shule ya sekondari Luganga tumeshapata vitendea kazi kutoka TCRA. Lakini pia nimeona kwenye bajeti Kata za Wambi na Bumilayinga zitapata minara. Ni kata muhimu kwa sababu Wambi ndipo yapo Makao Makuu ya Halmashauri na Bumilayinga tumejenga Kituo cha Afya, hivyo ni muhimu kupata mawasiliano. Aidha, TTCL wamekamilisha mnara katika Kijiji cha Itimbo, bado kuwasha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo nina maombi TCRA kwa ajili ya shule mpya ya sekondari ya Upendo ili tuwasaidie vitendea kazi vya TEHAMA.

Pia ninashauri kulitizama kwa ukaribu Shirika la Magazeti ya Serikali kwa kuwawezesha mtambo ili waweze kuchapa magazeti yao kwa rangi na hivyo kuwawezesha kushindana katika soko. Aidha, Managingi Editor anakaimu nadhani toka ambaye sasa ni Katibu Mkuu aondoke, Bi. Tuma Abdallah amekulia TSN, nadhani ni wakati sasa kumthibitisha ili kumpa morali na ufanisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu TBC Radio, wananchi wa Mafinga wanatamani mno kupata matangazo ya TBC lakini inasikika kwa taabu mno, hata redio nyingine hazisikiki, wananchi wa mji huu wa kibiashara kutokana na biashara ya mazao ya misitu wanaomba basi hata redio nyingine zisikike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TBC Tv kwa kweli kazi nzuri, ubunifu wa hali ya juu wa vipindi, nawapongeza.