Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia nimpongeze Katibu Mkuu pamoja na Naibu Katibu Mkuu na Msemaji Mkuu wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuendeleza mchango wangu kwa kuwashukuru TBC kutangaza Wilaya yangu ya Nyasa kupitia TBC1 na Safari Channel chini ya uongozi wa Dkt. Ryoba. Navishukuru pia vyombo vingine vyote vya habari kwa kuwa si rahisi kukitaja kila chombo vikiwemo vyombo vva habari mtandao (online).

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia uboreshaji wa mawasiliano katika Wilaya ya Nyasa, eneo la Kata ya Linga, Mbaha, Kijiji cha Ndonga na Njambe, Mpepo, Kihulunga, Ng'ombo na Mtupale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi maalum ni kuwa tulipata ufadhili wa kompyuta kwa ajili ya shule ya Tingi, lakini kutokana na mtandao kuwa chini mradi huo unataka kusimamishwa tumepewa miezi miwili tufuatilie uboreshwaji wa mawasiliano hayo. Aidha, Maafisa Habari wanafanya kazi kubwa lakini hawana vitendea kazi vya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.