Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Kwanza namshukuru Mungu kwa kunipa uhai na kuweza kuwa na afya njema kuweza kuhudhuria Bunge lako Tukufu. Pia nashukuwa nafasi hii kumpongeza Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan pamoja na Mawaziri wa Wizara ya Ujenzi na Manaibu na watendaji wote kwa kazi nzuri wanayoifanya, hakika wanajitahidi na kazi wanazichapa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Wizara ya Ujenzi jambo la kwanza linazungumzia mambo ya viwanja vya ndege. Kwa Mkoa wangu wa Lindi kuna viwanja viwili vya ndege kiwanja cha Lindi Mjini na Kiwanja cha Nachingwea. Viwanja hivi ni muhimu sana kwa kuwa Mkoa wa Lindi uko mpakani mwa Tanzania. Mikoa hii ya pembezoni ni muhimu sana barabara na viwanja vya ndege viwe vizuri kwa ajili ya usalama wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Kiwanja cha Ndege cha Lindi kiwekewa lami na Kiwanja cha Ndege cha Nachingwea kifanyiwe matengenezo kwa haraka. Pia kuna wananchi wengi wa Nachingwea walitoa viwanja vyao na maeneo yao Mei, 2018, wananchi hao walikuwa 107, kupisha mwendelezo wa viwanja vya ndege.

Mheshimiwa Naibu Spika, inasikitisha sana kwamba imepita miaka minne na huu unaingia mwaka wa tano wananchi wale hawajapewa haki yao, wananchi wale walikuwa wanalima pale, wanafanya mambo yao mengi ya maendeleo yao na haki zao za msingi zipo kwenye maeneo yale. Serikali wanaposhikilia maeneo yale mpaka leo miaka mitano haijawa-compensate wale wananchi kwa kweli hatuwatendei haki. Naiomba Serikali, najua Waziri wa Ujenzi na Naibu Waziri ni wachapa kazi, naomba walichukue hili wawalipe wananchi wale kwa maeneo yao waliyoyatoa kwa ajili ya kupisha viwanja vya ndege.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie masuala ya barabara. Ninapoongelea suala la barabara Mkoa wa Lindi naanza nachanganyikiwa sana. Mikoa mingi ya pembezoni tulisahaulika sana zaidi Mikoa ya Kusini, hilo nitaliongea wazi kama walivyokuwa wamechangia Wabunge wengine wa Mkoa wa Mtwara na wengine, Mkoa wa Lindi tulisahaulika katika barabara nyingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitoe shukrani kwa Wizara ya Ujenzi, kuna baadhi ya barabara tumeziona zimewekwa kwenye na bajeti, lakini kuna barabara zingine hatujaziona. Kuna barabara ya Njia Nne - Tingi kwenda Kipatimu, hii barabara ni kilomita 50. Hii barabara ni ya muhimu sana, inapita kwenye Milima ya Matumbi kwenye Pori la Akiba la Selous na ni ya kimkakati na barabara ile iko kwenye milima, barabara ni mbaya sana, kwa uchumi wa nchi yetu hii barabara ni muhimu kwa ajili ya utalii. Tunaomba barabara hii itengenezwa, imetegenezwa kilomita 1.4, sawa tunaishukuru Serikali, lakini bado kilomita 48.6. Tunaomba Wizara iiweke kwenye bajeti ili itengenezwe barabara hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitoe shukrani kwa Wizara ya Ujenzi, kuna baadhi ya barabara tumeziona zimewekwa kwenye na bajeti lakini kuna barabara zingine hatujaziona. Barabara ya njia Nne Tingi kwenda Kipatimo hii barabara ni Km 50, barabara ni ya muhimu sana inapita kwenye milima ya Matumbi kwenye pori la akiba la Selous hii barabara ni ya kimkakati na iko kwenye milima ni mbaya sana, kwa uchumi wa nchi yetu hii barabara ni muhimu kwa ajili ya utalii tunaomba hii barabara itengenezwa, imetegenezwa kilomita 1.4 sawa tunaishukuru Serikali lakini bado kilomita 48.6 tunaomba muiweke kwenye bajeti itengenezwe barabara hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia ni muhimu sana kwa kumbukumbu na Vita ya Maji Maji tunaomba muikumbuke. Pia kuna barabara nyingine ya Nachingwea - Nanganga kilomita 40, barabara hii ni muhimu lakini nimesikitika sana kwenye bajeti hii sijaona kutengewa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru barabara ya Nanganga kwenda Ruangwa - Nachingwea, Nachingwea - Masasi tayari imewekewa bajeti, kwa kweli niwashukuru sana Wizara ya Ujenzi. Barabara ya Nanganga - Nachingwea ni muhimu sana naomba muifikirie. Pia kuna barabara ya Nachingwea kwenda Liwale nikianza kuongelea hii barabara nachanganyikiwa, barabara hii ni kilomita 130 ni barabara mbovu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii barabara hata ikinyesha mvua ya dakika tano tu ile barabara uwezi kupita, barabara ile ni mbaya, barabara ile inakatisha tamaa, tunaomba mtukumbuke barabara ya Nachingwea - Liwale itengenezwe, barabara ile ni ya mkakati, kule Liwale kuna Kilimo kinaendelea, kuna Mbuga tunapita pale katikati, jamani tunaomba barabara hii ifikiriwe, barabara hii tunapiga kelele kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Nachingwea alishaiombea barabara hiyo sana siyo mara moja, Mheshimiwa Chinguile, Mheshimiwa Kuchauka amesema mara chungu nzima kuhusu hiyo barabara, jamani tunaomba barabara ile tutengenezewe, barabara ile ni muhimu na ni ya mkakati sana. Barabara hiyo wananchi wa kule kwanza hawaijuwi lami, tangia wamezaliwa na wengine mpaka wanakufa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna barabara zingine zilishatengenezwa lakini baadaye zimekuja kufanyiwa matengenezo mara ya pili, yaani zina lami lakini wanakwangua wanaweka lami ya pili, jamani Tanzania hii moja tufikiriane, jamani na sisi tuomba lami na sisi tunasikitika wananchi wetu kule hatujui lami, kama mnakwangua barabara zingine manarudia kuweka lami ya pili, kwa nini sisi hata ile barabara ya kwanza hamtuwekei lami jamani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wa Lindi, naomba mtufikirie sisi tulioko pembezoni, kwanza kuna Kambi za Jeshi kubwa za muhimu sana kwa ajili ya usalama zile kambi kubwa za Nachingwea Lindi kunatakiwa kuwe na barabara nzuri kwa kweli na viwanja vya ndege vizuri, suala lolote linaweza likatokea, kule ni mpakani bila kuwa na barabara nzuri ni changamoto jamani, kuna akina Mama wanafia njiani, watoto wanafia njiani kwa ajili ya barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi siyo mruka sarakasi wala mimi sifanya kitu, lakini najua Mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan ni msikivu naomba watufikirie watu wa Mikoa ya Kusini zaidi pembezoni huku Mikoa ya Lindi na Mtwara, barabara zetu hazipitiki jamani tunaomba. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Nachingwea kuna Kambi ya Jeshi na ile Kambi ya Jeshi imetunza Viongozi wengi wa Afrika.

NAIBU SPIKA: Ahsante, kengele ya pili hiyo.

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja lakini naomba mtufikirie barabara watu wa Mkoa wa Lindi. (Makofi)