Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon Toufiq Salim Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. TOUFIQ SALIM TURKY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa dakika hizo chache nilizopata. Kusema kweli nilikuwa sipo katika wachangiaji, lakini inabidi tuongee jamani kwenye ukweli. Mnyonge mnyongeni haki yake apewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, sote ni mashahidi kama dunia sasa hivi iko katika changamoto. Sote ni mashahidi kuwa sasa hivi bajeti iko katika constrain, lakini leo mbali baada ya kuisifu Wizara na Serikali ya mama wengi najua kila mmoja kupitia jimboni kwake tuna changamoto nyingi, lakini umepatikana muarobaini wake na muarobaini ni kitu gani? Mheshimiwa Waziri kaongea kama sasa hivi anakuja na EPC Plus Finance. Maana yake nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, kuwa leo hata kama bajeti haipo, basi leo tutafute huko nje watu, watakuja. Kuna miradi imewekwa kilometa 900 kwa ajili ya kuleta mkakati wa kusaidia Serikali. Kwa hivyo, niipongeze kwanza Wizara, hususan Waziri na timu yake kwa kuhakikisha wamekuja na wazo zuri zaidi kwa kuhakikisha wanaweza kuzi-finance hizi barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, halikadhalika naomba niongelee suala zima la ATC, ATC jamani karibuni tu nilikuwa na safari ya kibiashara kuelekea Kigoma. Mtu wangu akaniambia ili kufika Kigoma itabidi nimpatie posho ya siku mbili, nimpatie posho ya siku mbili, nimpatie na gari na mafuta kilometa elfu moja na zaidi. Nikamwambia hayo yote unataka bei gani? Akasema milioni tatu na service ya gari? Nikamwambia kwa nini usichukue tiketi ya ndege laki sita ukaenda ukarudi ukamaliza biashara?

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema ahsante kwa Wizara kwa kuhakikisha leo tunaifungua mikoani. Mikoa tunaifungua kwa kuhakikisha uchumi wa nchi unakuwa juu. Jamani lazima tupige na hesabu, sio kila time tutazame ndege inapata hasara gani, faida gani inapatikana. Tutazame ni biashara gani inapatikana kwa watu kuzunguka kwao na ile mikoa inafunguka vipi kibiashara? Huo ndio uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hivyo nafikiri kuna umuhimu sana wa Wabunge kufanyiwa semina ya kuweza kufahamu hili suala. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante kwa mchango mzuri, mengine andika.

TOUFIQ SALIM TURKY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ilibakia dakika moja lakini.