Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi hii. Mkoa wa Dar es Salaam ndiyo Mkoa ambao una network ndogo ya TANROADS kuliko nchi nzima, tuna barabara 51 za TANROADS urefu wa kilometa 601. Katika Jimbo la Ubungo ndilo lenye barabara chache cha TANROADS kuliko nchi nzima. Nimefanya hesabu kwenye mtandao wa TANROADS. Tuna barabara tano tu za TANROADS zenye urefu wa kilometa 28.8. Vile vile tunayo barabara moja ambayo imekuwa kitendawili kwa muda mrefu, inaitwa barabara ya Kimara – Kinyerezi; ikipita Kimara, Mavurunza - Bonyokwa hadi Kinyerezi, kilometa nane. Tangu mwaka 2010, Rais wetu wa nne aliahidi kwamba barabara hii itawekwa lami.

Mheshimiwa Spika, na kwa heshima yake ikaitwa Kikwete Highway mwezi wa pili mwaka huu kwenye Bunge hili niliuliza swali la nyongeza hapa kwa Mheshimiwa Naibu Waziri na akanijibu vizuri sana niliuliza barabara hii itaanza kujengwa lini? Mheshimiwa Naibu Waziri akajibu kwa furaha na kwa ushujaa mkubwa kwamba barabara hii ingeanzwa kujengwa na mwaka huu ingewekwa kwenye bajeti.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Engineer Kasekenya, nimeangalia kwenye bajeti ya Mheshimiwa Waziri nimeenda pale kilichonishangaza ni kwamba barabara hii miaka yote huwa inakaa kwenye kiambatisho cha 5(b)na kinakuwa sehemu ya A ambayo inakuwa ni barabara za lami safari hii imewekwa sehemu ya B ambayo ni barabara ya changarawe ama udongo.

Mheshimiwa Spika, sasa Mheshimiwa Naibu Waziri lile jibu lako liliibua shangwe pale Kimara, Kimara inawatu 118,000 ni sehemu muhimu sana Kimara ina baa peke yake 48 biashara rundo pale guest house 34, saloon 20, maduka rejareja 191, supermarket zipo 16 yaani pale ni eneo kubwa la biashara, watu wengi ikaibuka shangwe watu wakaanza kujiandaa kufungua biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa leo hii habari itasababisha mgutuko wa akili, mshtuko wa moyo na mtanziko wa kiroho, kwangu mwenyewe na kwa wananchi wa Jimbo la Ubungo na hususani Kata ya Kimara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hili jambo naomba Mheshimiwa Waziri ulieleze vizuri na ningesema hapa nishike shilingi lakini Mheshimiwa Professor Mbarawa alikuwa bosi wangu alikuwa Waziri wa Maji nikiwa Katibu Mkuu wake nilimsaidia akaupiga mwingi mpaka mama amemuona tena kwenye wizara hii nyeti sasa Mheshimiwa Professor Mbarawa mimi si nilikusaidia pale ukaupiga mwingi pale wewe hii barabara kilometa nane ukimsaidia Katibu Mkuu wako kuna ubaya gani? yaani kweli Katibu Mkuu wako ashike shilingi haiwezekani kwa sababu Mheshimiwa Mkuchika alishanifundisha kwamba once a boss always a boss wewe ni bosi wangu sasa nitashikaje shilingi yako. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hebu nisaidie hili peke yake tafadhali kilometa nane Kimara – Mavurunza – Bonyokwa – Kinyerezi watu 118,000 biashara chungu nzima wale wananchi walifurahi na nimeenda pale Kimara nimepokelewa kama mfalme nitaendaje sasa hivi? Nilikuwa napanga nikafanye mkutano wa hadhara nitafanyaje mkutano wa hadhara katika mazingira haya. Professor Mbarawa uniokoe bwana kauli yako tu hili linaisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho; katika Mpango Wetu wa Maendeleo huu wa Tatu bado miundombinu kipaumbele cha juu na kwakweli mahitaji ya barabara bado makubwa kama ambavyo tumeona kwa Waheshimiwa Wabunge hapa lakini mwaka huu labda Mheshimiwa Waziri utoe maelezo kidogo mwaka huu wizara Sekta ya Ujenzi bajeti imepungua mwaka jana ilikuwa 1.588 trillion mwaka huu ni trilioni 1.42 kwanini bajeti imepungua ya Sekta ya Ujenzi wakati Bajeti Kuu ya Serikali imepanda trilioni 37 mpaka trilioni 41 nadhani Mheshimiwa Waziri atupe maelezo.

Mheshimiwa Spika, na mwisho nichukue nafasi hii anapo ingia kiongozi mpya anakuwa na kazi kubwa tatu kwanza; ni kuendeleza yale mazuri aliyoyakuta; pili ni kurekebisha yale ambayo yalijitokeza changamoto ambazo hazifai kwa kipindi hicho na tatu ni kuleta mambo mapya. Mheshimiwa Rais wetu kwakweli aliahidi angehakikisha kwamba miradi yote mikubwa inaendelea na tuchukue nafasi hii kumshukuru sana kwasababu miradi yote muhimu inaendelea kama ilivyo na kwa kasi zaidi hili ni muhimu tumpongeze na tumshukuru sana kwa kazi kubwa ambayo anaifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumtie moyo kwamba hii miradi tupo naye na itasimama na niwahahakishie nimefanya kazi na Mheshimiwa Professor Mbarawa ni mtu ambaye kwenye miradi anajua kuisimamia ila tu wewe muhimu kabisa Mheshimiwa nakutia moyo lakini barabara yangu ya Kimara – Kinyerezi iangalie ni muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ahsante sana. (Makofi)