Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Awali ya yote ninamshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Manaibu Waziri wote wawili, pia nawapongeza sana Meneja wa TARURA Mkoa, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Arusha, vilevile meneja wangu wa Wilaya ya Karatu wa TARURA.

Mheshimiwa Spika, naishukuru Serikali katika bajeti ya mwaka jana 2021/2022 katika Jimbo la Karatu kulikuwa na wananchi ambao wamepisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Lake Manyara, lakini naishukuru Serikali katika mwaka huu, wamelipa wale watu kwa zaidi ya 5.9 Bilioni kwa maana wananchi wale wa Jimbo la Karatu wanaishukuru Serikali na mimi kama Mwakilishi wao pia naishukuru Serikali kwa malipo haya ya 5.9 Bilioni naamini kwamba tathmini ilifanyika mwaka wa 2014 na wananchi wale wamelipwa mwaka wa 2022 naamini pia kuna changamoto lakini kwa hili la kulipwa 5.9 naishukuru Serikali ya Chama cha Mapinduzi chini ya Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niseme katika Jimbo la Karatu kuna barabara hii ya Karatu - Mbulu - Hydom - Singida, lakini vilevile nilitaka niweke kumbukumbu sahihi Karatu iko Mkoa wa Arusha iko Mkoa wa Manyara, kwa sababu mara nyingi sana Manaibu Mawaziri wanapojibu kwamba wanaitafsiri barabara hii inaunganisha ikiwa ndani ya Mkoa wa Manyara barabara hii ya Karatu Mbulu - Hydom Singida ambayo ni Km 109 ambayo iko kwenye Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, mwaka wa 2010 chini ya Jakaya akiwa mgombea wa Uraisi wakati huo, 2015 Hayati Magufuli akiwa mgombea wa Chama cha Mapinduzi, mwaka 2020 ikiwa sisi kama wagombea wa Chama cha Mapinduzi wakati ule tuliaminishwa kwamba iko kwenye Ilani ya uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi na wakati wowote hii barabara inaweza kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, changamoto na ngonjera zimekuwa nyingi kupitia Wizara hii ya Ujenzi kwamba mwaka jana tuliambiwa imetengwa Km 25 na mwaka jana walisema wamekosa Mkandarasi aliyeomba kwa Km 25 umeongeze 25 sasa jumla ni Km 50, ambayo itaanzia Mbulu- Hydom, lakini tulifikiri ingeanza tungeshukuru lakini mpaka sasa hivi ipo kimya giza nene. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, barabara hii ni ya Km 190 kama alivyoelezea mwezangu ambaye jana alitaka kuruka sarakasi sisi wengine hatuwezi tunaweza kuiseme tu Serikali kwa lugha nzuri na mtuelewe kwamba Wilaya Saba ambayo inaunganisha na ile barabara ya Karatu, Mbulu, Hydom, Singida na maeneo mengine ya Wilaya mbalimbali ndani ya Mkoa wa Singida.

Mheshimiwa Spika, kuna barabara nyingine ambayo ni barabara ya Karatu, Mangola, Matala ambayo inaunganisha Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu. Ni nia ya Serikali kwamba sasa hizi barabara za kuunganisha Mkoa, kwa mfano kwa sasa Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu bado haujaunganishwa na barabara hiyo ni ya urefu wa Km 328, lakini naamini Wabunge walio wengi ni Wabunge wanaotokana na CCM, tulitembea kwa wananchi wa Tanzania tukiwaaminisha kwamba Ilani hii ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ndani ya miaka mitano tunaweza kwenda kuitekeleza.

Mheshimiwa Spika, naamini sasa tuna takribani miaka miwili utekelezaji katika Jimbo langu kuanzia sasa ni asilimia Sifuri sasa nafikiri imebaki miaka miwili na chenji, je Ilani ile ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ambayo tumewaaminisha Watanzania walio wengi na walioko ndani ya Jimbo la Karatu. Mheshimiwa Waziri tukuombe, kwa sasa changamoto ni kubwa tunajua lakini tuamini kwamba sasa tutathmini kwa miaka hii miwili Je tumeweza kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi 2020/2025 kwa kiwango gani ndani ya miaka hii miwili ili mwaka mwingine unaokuja wa fedha tuweze kuona ni namna ipi tunaweza kuweka vizuri Ilani yetu isituletee shida kwa wananchi wetu ambao tunawaongoza na wametupa kipaumbele tuwasemee katika jengo hili Takatifu.

Mheshimiwa Spika, niseme Km 328 kuunganisha barabara ya Mkoa wa Simiyu na Mkoa wa Arusha siyo kilometa nyingi sana, naamini barabara hii itakuwa ni barabara fupi ya kuunganisha Mkoa wa Shinyanga kwenda kuunganisha Mwanza na Mikoa mingine ya huko kama Mkoa wa Mara na Mikoa mingine ya ukanda wa Ziwa. Tunaomba Serikali Km 322 ambayo inaunganisha kibiashara Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu.

Mheshimiwa Spika, mwaka wa 2015 tulitembelewa kwa wakati huo alikuwa Makamu wa Rais, leo ni Rais alisema kuna barabara ambayo alituahidi kwa kipindi hicho kwa kiwango wa lami, mwaka 2015 barabara inayotoka Kibaoni inaelekea Endabashi siyo kubwa sana kilometa zake lakini barabara hiyo hata siyo kwa kiwango cha lami tunaomba iwekwe hata kwa kiwango cha moram.

Mheshimiwa Spika, ahsante naunga mkono hoja. (Makofi)