Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi kuweza kuchangia kwenye Wizara hii ya Ujenzi na Uchukuzi. Kwanza ninatoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yote ya Watendaji kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya, wakazi wa Mkoa wa Tabora tunashukuru sana kupata lot ya ujenzi wa treni ya umeme tunasema ahsante sana muendelee kuupiga mwingi kama ambavyo mmekuwa mkiupiga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mchango wangu kwanza nimpongeze mwalimu wangu ambaye ni Mkurugenzi wa LATRA Mheshimiwa Richard Ngewe huyu ni Mwalimu wangu na amenifundisha Chuo, amekuwa anafanya kazi nzuri toka tukiwa chuoni, pia hata katika kazi zake za utumishi. Ninakuomba Mheshimiwa Waziri akiwa anaelekea kustaafu basi umwangalie vizuri ni Mwalimu mzuri na amefanya kazi nzuri, amepewa kusimamia LATRA na sisi watu ambao tumesomea masuala ya sekta ya usafiri na uchukuzi, Mheshimiwa Waziri tunatambua sekta hii ya usafiri na usafirishaji inahitaji watu waliobebea kwenye sekta hii, nikuombe uwezeshe hii taasisi ya LATRA iweze kufanya kazi zao vizuri, hasa katika kitengo cha ukaguzi tumeona ukaguzi wa magari imekuwa ikifanywa wakati mwingine na polisi nikuombe kuna vijana wengi sana wamesomea usafirishaji katika vyuo special wapewe hizi kazi wazifanye kwa sababu ndiyo professional yao tofauti na kuwapa polisi wahifanye hii kazi maana yake unawaondoa watu ambao wamesomea by professional na unawapa kazi ambayo badala ya kusimamia sheria wanafanya kazi zingine tena, ninakuomba vijana hawa waliosomea logistics wafanye kazi hii ya ukaguzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri kwa Professional nimesomea Logistics and Transport Management ninaifahamu vizuri sekta hii ya usafiri na usafirishaji, ninakuomba sana uweze kuwaangalia hawa vijana. Pili ninakuomba Mheshimiwa Waziri kuna Bodi ya Usafirishaji, hatuna Bodi mpaka hivi sasa lakini kuna maombi ya kuwepo kwa Bodi ya Usafirishaji nikuombe sasa sijui imefikia wapi hii Bodi, Mheshimiwa Waziri tunaiomba hii Bodi kwa ajili ya ufanisi katika kuinua sekta ya uchukuzi kwa uchumi wa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri sekta ya uchukuzi ni muhimu sana katika kuinua uchumi wa Taifa letu nikuombe sana sekta hii au bodi ya usafiri na usafirishaji tuweze kuipata kwa wakati. Ninajua ipo kwenye pipe line lakini naomba muisukume ili tuweze kuipata kwa haraka na tuweze kuokoa sekta hii ya usafirishaji.

Mheshimiwa Spika, lingine ninakuomba Mheshimiwa Waziri ATC ina madeni mengi sana, ninaomba yale madeni ambayo watu wametoa service kwenye Shirika letu la Ndege waweze kuwalipa wadau, madhara yake kutokuwalipa ni kurudisha nyuma juhudi za Watanzania. Mheshimiwa Waziri lipeni madeni ATC walipe madeni hilo pia nilitaka kuchangia.

Mheshimiwa Spika, lingine ninakuomba Mheshimiwa Waziri, wewe unafahamu tunaomba barabara, Jimboni kwetu Manoga Wilaya ya Igunga barabara inayotoka Choma kuja Ziba kuja Nkinga mpaka Puge kuelekea Tabora, hii ni barabara muhimu iliahidiwa na Hayati Rais Dkt. John Pombe Magufuli kipindi cha kampeni 2015, pia iliwekwa kwenya ahadi ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi….

SPIKA: Muda wako umeshaisha Mheshimiwa.

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Spika, Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020 kwa hiyo nakuomba Mheshimiwa Waziri utupatie barabara hiyo.