Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Bahati Khamis Kombo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO: Mheshimiwa Spika, mchango wangu zaidi utagusa sekta ya bandari.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali kufanya utaratibu kuongeza vifaa vya kushushia makontena. Pia kuna vijana ambao walishiriki ujenzi wa meli MV Mwanza, vijana wale nakuomba Mheshimiwa Waziri kuwaangalia kwa jicho la huruma pindi ikimalizika kama kutakuwa na ajira basi uwape kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, tumejenga barabara nyingi, naomba sana tusisubiri mpaka zikaharibika, tukiona ishara tu ya dosari basi tufanye matengenezo.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.