Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa pongezi kwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Naibu Mawaziri na watendaji wakuu wa Wizara kwa kazi nzuri ambayo wameendelea kuwafanyia Watanzania.

Napenda kumshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha ambazo zilifanikisha ujenzi wa barabara ya lami kutoka Loliondo_Sale (kilometa 50). Kwa kuwa barabara hii ni muhimu kwa uchumi wa Wilaya ya Ngorongoro kwa ajili ya kuunganisha Wilaya ya Ngorongoro na Mkoa wa Arusha.

Kwa kuwa Waziri alishaagiza TANROADS kutangaza kilometa 50 zingine, naiomba Wizara iharakishe mchakato huo wa kutekeleza mradi huo wa kilometa 50 kutoka Sale - Ngaresero na baadaye kutoka Ngaresero mpaka Mto wa Mbu. Barabara hii itasaidia kufungua uchumi ya Wilaya ya Ngorongoro huku tukifahamu kuwa Wilaya yetu ya Ngorongoro ina vivutio vingi vya utalii na ili kurahisisha ufanyaji wa biashara ya utalii na watalii kufika kwenye vivutio hivyo, ni muhimu sana barabara hii kutengenezwa.

Mheshimiwa Spika, Wizara pia itenegeneze fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi wa barabara ya lami Makao Makuu ya Wilaya ya Ngorongoro eneo la Wasso - Loliondo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.