Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Makame Mbarawa - Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi pamoja na Naibu Mawaziri wote wawili. Pia nampongeza Katibu Mkuu Engineer Asha na Naibu Makatibu Wakuu kwa kazi nzuri. Naomba pia nimpongeze Meneja wa TANROADS Ruvuma, yupo imara. Nawapongeza pia Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari - Ndugu Erick Hamish na Mkurugenzi wa Shirika la Reli - Ndugu Masanja Kadogosa kwa semina waliyotupa ilituongezea uelewa wa kutosha kuhusu kazi nzuri zinazofanyika.

Mheshimiwa Spika, nina maombi yafuatayo; kwanza ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara za Kitai hadi Lituhi na hadi bandari mpya ya Ndumbi; Mbamba Bay hadi Lituhi; na kukamilisha upembuzi yakinifu/wakina Nangombo hadi Chiwindi.

Mheshimiwa Spika, pia ujenzi wa Daraja la Mitomoni; kuanza upembuzi yakinifu barabara ya Noni, Kingerikiti, Tingi hadi Mitomoni; kujenga barabara ya Likuyufusi hadi Mkenda na kuunga Daraja la Mitomoni.

Mheshimiwa Spika, tunaomba boti la fibre ya kutosha tani mbili ili kuvusha watu na mizigo yao wakati tunasubiri ujenzi daraja la Mto Ruvuma (Mitomoni). Aidha, Wizara itenge fedha za kutosha kwa ajili ya matengenezo ya kina kwa kiwango cha changarawe na strips za zege kwenye maeneo korofi. Wilaya ya Nyasa ina milima na mvua nyingi.

Mheshimiwa Spika, pia kuboresha bandari na majengo ya bandari ikiwemo kuweka navigation marks kwa ajili ya kuongozea meli. Ujenzi wa Reli ya Mtwara hadi Mbamba Bay pia hadi Mchuchuma na Liganga.

Mheshimiwa Spika, kimataifa meli za Ziwa Nyasa ziweze kwenda hadi Malawi tufanye biashara. Pia kasi iongezwe ya kuwezesha usafirishaji wa mizigo baina ya Tanzania na DRC bila kulazimika kupitia nchi nyingine.

Mheshimiwa Spika, iko haja ya kuchochea fursa katika maeneo yaliyoachwa.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.