Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa Duniani na kupewa Tuzo ya mafanikio ya ujenzi wa miundombinu

Hon. Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa Duniani na kupewa Tuzo ya mafanikio ya ujenzi wa miundombinu

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kwanza nikushukuru kwa kunipa heshima, hii ni heshima kubwa ambayo kwa kweli sikuidhania wala sikuiamkia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nianze kwa kusema kwa niaba yangu lakini kwa niaba ya Wabunge wenzangu, kwamba Mama sisi kama Wabunge tunakupongeza sana sana sana. Kwa kawaida upo msemo wa Kiswahili unasema hakuna Nabii aliyewahi kupendwa kwao lakini mama sisi wenzako, Wabunge wenzako tunakupenda, tunakuthamini sana sana sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na kwenye hili nadhani ipo nafasi ya sisi kama Wabunge lakini sisi kama taifa kuanza kujitathimini upya kwasababu si lazima tusifiwe na wengine tunayo nafasi ya kujisifu na kusifu vya kwetu. Mheshimiwa Rais amefanyakazi kubwa, Mheshimiwa Rais anafanyakazi kubwa tunaiona, tunaithamini. Kwa hiyo, tunaomba tukupe moyo ili uendelee kufanya mema zaidi ili watanzania waendelee kufaidika kwa kuhakikisha kwamba unawaondoa walipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa maana yangu ni nini, zawadi au chombo hiki kilichotolewa ni kuashiria kazi kubwa aliyoifanya na anayoifanya mama kwaajili ya maslahi ya taifa lake. Mimi ningeomba mama yetu asirudi nyuma na sisi wabunge kwa kushirikiana na wananchi tuendelee kumpa moyo ili aone kwamba bado anahitajika kufanya mambo mazuri zaidi. Asiogope mama yetu kwasababu atakapofanya jema na sisi Wabunge tukaliona, tukamuunga mkono maana yake hili ndilo ambalo Watanzania wanalolitegemea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naomba niseme kwa ufupi hivi, kwamba kwasababu dunia imeona, kwasababu Afrika imeona, kwasababu Wabunge wenzangu mmeona maana yake ni nini, ni kuonesha kwamba mama yetu tokea ameteuliwa kuwa Makamu lakini pia kuteuliwa kushika nafasi ya chombo hiki kama taifa maana yake amekubali kuendeleza yale yote waliyoyapanga na yanakwenda mbio na hayasimami. Kwa hiyo, ningeomba sana sisi tumpongeze kwa kauli moja kama tulivyofanya lakini tumpe nguvu tukimuambia kwamba tupo pamoja na yeye, tutafanya naye kazi na hakika hatutamuangusha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nikushukuru kwa nafasi, lakini ningeomba niseme ni yeye pamoja na mawaziri wake lakini kwa kusaidiwa zaidi na Mheshimiwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Rais wa Zanzibar naye, kwasababu haya wanayafanya kwa umoja wao. Kwa hiyo, zawadi hii imetolewa kwa viongozi wetu wote ambao wanasaidia kuliongoza taifa hili. Nawapongeza, nawashukuru sana sana, ahsante. (Makofi)