Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa Duniani na kupewa Tuzo ya mafanikio ya ujenzi wa miundombinu

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa Duniani na kupewa Tuzo ya mafanikio ya ujenzi wa miundombinu

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi napenda kutumia nafasi hii kwa niaba yangu mwenyewe na kwaniaba ya wananchi wa Mafinga kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa tuzo hii ambayo anaipata, akiwa ni kiongozi wa 12 katika Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuzo hii haitolewei tolewi tu, inatolewa kwa mtu ambaye kwanza amethibitisha dhamira yake katika kuendeleza miundombinu ya usafirishaji, hili si jambo dogo. Miundombinu ya usafirishaji na kuaminika huku kwa Mheshimiwa Rais kwanza kunalijengea taifa letu heshima lakini pia kunalijingea taifa letu kuaminika na kuaminiwa na vyombo vikubwa vya kimataifa duniani. Kama ambavyo tumeona, tuzo hii imetolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika, na tunafahamu mchango wa Benki ya Maendeleo ya Afrika katika ujenzi wa miundombinu katika taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwakutoa tuzo hii kwa Mheshimiwa Rais wetu si tu kwamba tunaendelea kuaminika katika Benki ya Maendeleo ya Afrika lakini pia tunaendelea kuaminika katika vyombo vingine vya fedha duniani. Kwasababu kama ambavyo tumeona kwenye bajeti yetu juzi kila Mbunge aliyesimama kilio kikubwa kilikuwa ujenzi wa barabara na kikubwa kilikuwa resource hazitoshi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa kuaminika na kwa kupata tuzo hii kwa kuheshimishwa kiasi hiki maana yake ni kwamba sasa kama taifa hata tunapoenda kuomba kama ni grants hata kama ni mikopo ya riba nafuu kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya taifa letu tutaweza kuaminiwa na kuaminika. Na hivyo, kwa kujenga miundombinu hiyo maana yake ni kwamba tutaweza kusafirisha bidhaa zetu kwa namna nyepesi, tutaweza kusafirisha mbolea zetu kuwafikia wakulima kwa namna nyepesi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, itoshe kusema kabisa kwamba kama taifa, kama wabunge na kama Watanzania tujionee sifa kwa kuwa na kiongozi ambaye katika Afrika pekee mwaka huu ameenda kupewa tuzo hiyo. Ninaamini kabisa hata wana-Mafinga hapa ninapozungumza kuna ujenzi wa barabara zinaendelea pale Mafinga ni matokeo ya heshima hii ambayo tumepewa. Kwa hiyo, naunga mkono azimio hili na Mungu ambariki Rais wetu Mungu abariki Taifa letu. (Makofi)