Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana kwa kunipa nafasi.
Mimi kwanza kabisa naomba niseme kwamba ni Mjumbe wa Kamati ya Mindombinu na naomba kabisa nianze kwa kuunga mkono taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wetu Mheshimiwa Dkt. Norman Sigalla na pia naomba nianze kusema kwamba mimi naunga mkono hoja ambayo iko mbele yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, amejitahidi kadri alivyoweza, lakini na sisi kazi yetu hapa ni kuboresha. Kwa hiyo, naomba nizungumze kwa mtizamo huo wa kuboresha yaani positive and forward looking contribution. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi iliyo mbele yetu ni kubwa. Nimewahi kusema na kila nitakaposimama nitarudia, kwamba nchi yetu imebarikiwa, tumepata kiongozi ambaye sasa anatuingiza katika mapambano mapya ya kupigana na umaskini. Umaskini huu unamaanisha kwamba tunasomesha watoto, lakini watoto hawawezi kupata ajira kwa sababu hatujajipanga vizuri kuweka miundombinu ambayo itaweza kubadilisha hali yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri na pia cabinet nzima, Baraza la Mawaziri na Mheshimiwa Rais kwa kuona kwamba, sekta hii sasa ipewe angalau asilimia 16 ya bajeti ya Serikali. Lakini Kamati yetu ilipendekeza na niomba nisisitize kwamba hazitoshi na ushahidi kwamba hazitoshi Waheshimiwa Wabunge wote mnaposimama kila mmoja unaona kwamba, anasema mambo ya msingi ambayo ni pungufu. Barabara zinatakiwa zijengwe maeneo mbalimbali nchini kote na kila mmoja wetu hapa anastahili. Anastahili reli, reli inatakiwa kwenda katika kila Wilaya, anastahili bandari, lazima ziwe kila mahali na kadhalika, lakini sasa bajeti haitoshi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi mchango wangu nataka kusema kwamba wananchi wa Muleba Kusini ambao wamenituma hapa kwa mara nyingine na wenyewe wana matarajio yao. Matarajio yao ni kwamba, Hospitali yetu Teule ya Rubya, Hospitali ya Wilaya, iko milimani na huwezi kuifikia bila kupita Mlima wa Kanyambogo. Kwa hiyo, siwezi kurudi nyumbani kwa wananchi wa Muleba Kusini kwa kujiamini kama sijaweza kuwahakikishia kwamba Mheshimiwa Waziri utakaposimama utatwambia hatima ya barabara ya lami kutoka Muleba kupita Kanyambogo kwenda Hospitali Teule ya Rubya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa ridhaa yako nimkabidhi Mheshimiwa Waziri tender iliyoitishwa na TANROADS chini ya Waziri wetu wa Ujenzi wa zamani ambaye sasahivi anaongoza nchi ambayo ilikuwa kwenye Gazeti la Daily News la tarehe 13 Septemba, 2013. Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa Waziri wa Ujenzi aliitisha tender ya kujenga barabara ya lami kutoka Muleba kupitia Kanyambogo kwenda Rubya. Nimeona sasa hivi Mheshimiwa Waziri hujasahau kabisa, lakini umeweka kwamba ni ya changarawe. Kwa mlima wa Kanyambogo kuweka changarawe pale ni kutwanga maji kwenye kinu. Unaweka kifusi asubuhi, jioni kimeshaporomoka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati yetu imeshauri kabisa kwamba pamoja na ukosefu wa fedha TANROADS wajitahidi kuachana na mambo ya changarawe na kokoto, hawa ni watu wa lami ni watu wa viwango, watusaidie; sisi kazi yetu ni kuwatafutia fedha wanazostahili. Kwa hiyo, nataka kusema kwamba jambo hili ni muhimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sasahivi Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, amemaliza kazi yake. Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli wakati akiwa kwenye kampeni pale Muleba alituahidi na mimi naamini ni mtu wa ahadi, kwamba sasa hili litatekelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, sisi wanawake wa Tanzania tunajivunia sana na tunampongeza sana Mheshimiwa Samia Suluhu na alipopita Muleba akiwa kwenye kampeni aliahidi barabara ya lami kutoka Lunazi kwenda Ziwa la Burigi. Ziwa la Burigi ni ziwa (unique) la kipekee katika nchi yetu, lakini amini usiamini miaka 55 baada ya Uhuru hakuna barabara yoyote inayokwenda Ziwa Burigi ambalo ni unique ecosystem. Kwa hiyo, naomba kabisa hili nalo liangaliwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sasa kwa mchango wangu naweza nikasema mambo mengi. Watu wamezungumzia meli nimeshazungumza, kiwanja cha ndege cha Omkajunguti kuikomboa Kagera kutokana na umaskini imeshazungumzwa, naomba nikazie. Lakini pia kama mtu ambaye ninatoka Kanda ya Ziwa, reli ya kati imezungumziwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tunapozungumza reli tuangalie sasa kumuwezesha pia Waziri wetu…
WENYEKITI: Ahsante.