Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa Duniani na kupewa Tuzo ya mafanikio ya ujenzi wa miundombinu

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa Duniani na kupewa Tuzo ya mafanikio ya ujenzi wa miundombinu

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nami nichukue fursa hii kwa kweli kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tuzo hii aliyoipata. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mimi ni Balozi wa Afya ya Akili, nitaomba nitumie mfano ili watu waelewe, kwa sababu kuna watu wengine huwa pia hawaelewi. Mimi niseme hivi, hii tuzo ni kama kombe ambalo huwa zinacheza ligi zetu humu ndani ya nchi. Hapa hii tuzo ilikuwa inagombaniwa na nchi 54. Nchi zote za Bara la Afrika na wachezaji walikuwa ni Wakuu wa Nchi kwenye timu hizo, lakini aliyekuwa kashikilia tuzo hii ilikuwa ni wenzetu Nigeria. Kwa hiyo, naweza nikaendelea kutoa mfano; nichukulie kama Nigeria ilikuwa ni Yanga na Mama Samia ni Simba; wameingia kwenye fainali. Zilikuwepo sheria, kama zilivyo sheria 18. Hapa kamati ile ikaangalia, maana kuna watu hawaelewi wanafikiri labda imetolewatolewa tu kwa sababu ya hivi hivi, hapana. (Makofi/Kicheko/Kigelegele)

Mheshimiwa Spika, jambo mojawapo Mbunge mwenzangu aliyemaliza kusema ameshamaliza. La kwanza, ilikuwa wameangalia shilingi milioni 290 ambazo Tanzania tume-qualify kwa vigezo kupewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa ajili ya kuendeleza miundombinu chini ya usimamizi wa Rais Samia Suluhu Hassan, tukashinda kwa vigezo, tukaonekana tunafaa kupewa fedha hiyo kwa ajili ya kuendeleza miundombinu ya barabara, reli na usafiri wa anga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ya pili ikaangaliwa maono yetu baada ya kuwa tunajenga reli, tutai-manage vipi? Tutaiendeleza vipi? Tukaingia mkataba na kampuni nyingine ya China kutupatia modern flit cars kwa ajili ya kuendeleza sekta hii ya reli ambapo tutakuwa na magari 1,430 kwa ajili ya kusimamia uendelezaji wa sekta hii ya miundombinu ya reli. Hii iligharimu karibu dola milioni 172.2. Hayo ndiyo tuliyomtoa knockout Nigeria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ya tatu, ikaonesha nia ya Serikali ya Rais Samia; nimewahi sikia tetesi tetesi kwamba ule Mji Mkuu wa Nigeria, Abuja ule ramani yake inafanafana na masterplan ya Mji wa Dodoma. Sasa wao wamejenga ule Mji lakini walishindwa kwenye ring road hawajafanya. Sisi Tanzania tarehe 11 Februari, Rais wetu amezindua na kuanza rasmi ujenzi wa ring road katika Mji wetu wa Dodoma. Hiyo moja ilikuwa ni credit. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ndugu zangu Watanzania tunaposema Mama anafanya kazi kubwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hata vitabu vya Mwenyezi Mungu vinasema, wakati mwingine Nabii hapati heshima kwao. Ila mimi kama Balozi wa afya ya akili, naweza nikasema ni matatizo pia ya afya ya akili kutotambua kwamba una kitu cha thamani au una kiongozi bora ndani ya nyumba yako na kubeza juhudi za mama anapotoka kwenda kutafuta chakula; au baba anapotoka kwenda kupambana na maisha ili arudi na kitu kuendeleza familia. Ile nayo ni matatizo ya afya ya akili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ndugu zangu mama anapokuwa katika harakati za kuwepo ndani ya Tanzania, au anapokuwa katika harakati za kuwepo nje ya nchi ya Tanzania, ni kwa maslahi mapana ya Taifa letu. Leo hii katika hiyo fedha kila Mbunge hapa alipewa shilingi milioni 500 na wengine wamepewa shilingi bilioni moja. Leo hii nikifika Iringa, nikienda katika Kata yangu ya Mkimbizi pale, Namtivila kuna barabara tumejenga ambayo tumepeleka shilingi milioni 500 kutoka katika mgao huu. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa, kengele imeshagonga, ahsante sana.

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa hiyo, nawaomba ndugu zangu tumuunge mkono mama, anaupiga mwingi!

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)