Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa Duniani na kupewa Tuzo ya mafanikio ya ujenzi wa miundombinu

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa Duniani na kupewa Tuzo ya mafanikio ya ujenzi wa miundombinu

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja iliyotolewa na Mheshimiwa Zainab Katimba kufuatia tuzo aliyoipata Mheshimiwa Rais kwenye kuimarisha au kujenga miundombinu.

Mheshimiwa Spika, nikushukuru na wewe kipekee kwa kutaja jina langu na baada ya kulitaja ukanitamka nikiwa wa mwisho, matokeo yake nitakachosema hapa ni meseji nilizotumiwa na Wanajimbo wa Wilaya ya Muleba kwa ujumla na nyingine nimekurushia wewe.

Mheshimiwa Spika, Muleba wanasemaje kwenye tuzo hii? Wanasema jema lolote, lililoshindikana katika nchi hii sasa kwa Mama litalekelezwa, hiyo ni Muleba, jema lolote katika nchi hii lililofikiriwa na likashindikana kutekelezwa kwa Mama litatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, Muleba ni kubwa mno, wanasema Mheshimiwa Rais sio kwamba amejenga barabara, amejenga barabara kule ambako watu hawakufiria. Ukienda kule Muleba kule ambako watu hawakufikiria, alipopaona Mjerumani Muleba kuna barabara, amejenga barabara katika Kata ya Kamachumu na Luanga kupita Kyaraburamula ameshuka akaenda Chuo cha Elimu Katoke akajenga barabara mpaka ziwani Kamugaza. Wanasema Muleba, amejenga madaraja, barabara ya Kyamyolwa kwenda Kimeya, Kumuliza mpaka Kashebuko amejenga barabara. Kimbugo amejenga barabara, Mheshimiwa Rais amejenga barabara Kakindo mpaka Maziba, Mayondwe mpaka Bugasha, Muramura na Kyamyolwa. Mama anafungua barabara anakwenda kule ambako watu hawakufikiria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, amejenga barabara kwenda Ngenge zaidi, wameniambia mama, wanavyosema ni wagandagaza, wagandagaza maana yake nini ukimuona mtu analia, ukampangusa machozi, unaitwa uwagandagaza. Anajenga barabara kwenda Rutoro, kwenye Kisiwa cha Bumbile, mama anafanya mambo tofauti lakini yaleyale yaliyozoeleka. Wananchi wa Muleba na Kagera kwa ujumla wanampongeza na wanasema mama isifike mwezi Oktoba hujafika, haya matatizo madogo madogo ya ardhi yatakuwa yanakuja, uje tusherehekee, wamkumbuke Baba wa Taifa wakati anasema Mwenge.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi/Vigelegele)