Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, nashukuru nikiongezea kwa hoja ya Mheshimiwa Mhagama kuhusiana na eneo la Bunge, nakumbuka wakati wa hotuba ya Waziri Mkuu, Kamati ya Bajeti ilieleza suala hili kwa kina na tukaambiwa kwamba hoja hii imepelekwa Wizara ya Ardhi, kwa mantiki ya dhamira ya kutwaa maeneo. Sasa nilikuwa nadhani kwa sababu Wizara yenyewe mko hapa ni wakati muafaka wa kulitolea majibu hili ili kama kuna namna ya hatua za ziada kama ambavyo imependekezwa na Mheshimiwa Mbunge, iweze kufanyika kwa haraka, kwa sababu siku hazigandi na thamani ya ardhi inapanda kila siku kwa hiyo lazima uamuzi ufanyike na ufanyike haraka kwa maslahi mapana ya Taasisi ya Bunge lakini na wananchi kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili jana nilisikiliza kwa makini Wizara ya Mifugo, migogoro ya ardhi ilizungumzwa ikashikwa Shilingi hapa ikapigwa juu kwa juu kimtindo, lakini dhamira ilikuwa ni kuwapa somo wajifunze tunakoelekea inakuwaje. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo nikisoma hotuba ya Waziri, migogoro ya ardhi vilevile imezungumzwa na Waziri anasema kabisa kwamba katika mwaka 2021/2022 walitarajia kutatua migogoro 1,000 lakini wakatatua migogoro 1,800. Sasa ukimsoma nae Waziri wa Mifugo jana anasema alifanya mikutano 28 kwa ajili ya kutatua migogoro baina ya wafugaji na watumiaji wengine, yaani ni kama vile kutatua migogoro ni sifa. Mawaziri wameacha kufanya shughuli zao za msingi wanaenda kutatua migogoro. Tumesikiliza taarifa ya Kamati ya Ardhi imesema…

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY NDERIANANGA): Mheshimiwa Spika, taarifa.

TAARIFA

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY NDERIANANGA): Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kumpa taarifa Mheshimiwa Dada yangu Halima Mdee kwamba kati ya majukumu mengine ambayo Waheshimiwa Mawaziri walipewa, wamepewa kwa mujibu wa kanuni na utaratibu waendelee kufanya zoezi hilo. Kwa hiyo, asiseme kwamba wameacha majukumu yao ni kati ya sehemu ya majukumu yao kufanya shughuli hizo. Ahsante. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Halima Mdee, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. HALIMA J. MDEE: Siwezi kuipokea, mdogo wangu alitakiwa asubiri kwanza niendelee ajue najengaje hoja. Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati amesema hapa, kuna tatizo kubwa sana la kibajeti kwenye Tume inayowajibika kupanga nchi. Hili tatizo tunalizungumza leo kwa sisi wakongwe ni mwaka wa 15, sasa Mheshimiwa kama tusipojua principle moja kama Taifa, wananchi tunaongezeka ardhi haiongezeki. (Makofi)

Mheshimiwa kwa takwimu za Wizara yenyewe wakati tunapata uhuru mwaka 1961 watu walikuwa Milioni 10.3, ukigawa maeneo ambayo tunatakiwa tutumie ukiacha hifadhi na mambo mengine, ilikuwa gawio la ardhi kwa kila mtu ni wastani wa eka 8.4 mwaka 1961. Sensa 2012 tunaambiwa tulikuwa Milioni 43, kwa takwimu ya ardhi gawio ni hekta Mbili kwa kila mmoja tunazidi kudondoka, leo tunaenda sensa 2022 possibly ya Watanzania kufika Milioni 100 ni kubwa tutafika wapi? Mipango ya matumizi bora ya ardhi mifugo tunazungumza migogoro ya mifugo na wakulima, tunaambiwa 1978 tulikuwa tuna mifugo Milioni 21, mwaka 2012 tuna mifugo Milioni 43. Jana nimejumlisha kwa mujibu wa Waziri wa Mifugo ukichanganya ng’ombe, kondoo, mbuzi, kuku na kitimoto tuna jumla ya mifugo 1,165,000. Ninasema hivi nchi square meter ni zile zile square kilomita zile zile 945,000 lakini tume-shift from 10 Milioni Mungu anajua sensa itatuambiaje.

Mheshimiwa Spika, tume-shift from 20 and so now tuko 1,165,000, tunaambiwa hapa tumepitisha sisi wenyewe mpango wa miaka mitano, Tume yetu inahitaji Bilioni 15 tu kwa mwaka kuweza kufanikisha baada ya miaka mitano tuweze kupima vijiji 6,160. Bilioni 10 hivi leo kweli eneo hili muhimu ambalo tumejipangia kupima vijiji 719 kila mwaka tutimize target ya miaka hivi hatuna Bilioni 10? Halafu mnatuambia kwenye hotuba zenu hapa eti mnapiga maziara hivi hizo ziara mlizozipiga nyie wakubwa, tokea tumeanza kutatua migogoro ya ardhi nchi, hii hivi mmetumia shilingi ngapi? Au kwangu mimi kwa tafsiri yangu tu ya kawaida, ni hivi migogoro ya ardhi tunatumia kama dili kimtindo na kuweza kupata shughuli za kufanya.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu huwezi kuniambia tunakosa 10 Bilioni ambayo mimi nahakika Lukuvi pale kwa uzoefu wake, kwenye akaunti yake ana Bilioni 10 kama mimi ninayo kidogo dogo yeye anakosaje? Kwenye eneo ambalo tunatakiwa, nasema na nasisitiza kama kuna eneo ambalo tunaiomba Kamati ya Bajeti on a very serious note iende ikaliangalie katika mtindo huo huo wa maeneo ya Bunge tuliozungumza, kama tunaweza tukaenda tukafanya mambo ninaomba tumsaidie Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, najua Waziri anaandika lakini anachekelea si tunamtafutia hela, tumsadie Waziri apate Bilioni 10 tuondokane na matatizo ya migogoro ya ardhi nchi hii, wananchi wetu wanateseka, wakulima wanateseka, wafugaji wanateseka, lazima tuonyeshe leadership for once, haiwezekani Mkapa akashughulikia migogoro, Mzee wetu Mwinyi kashughulikia migogoro, Kikwete kashughulikia migogoro, Marehemu Magufuli kashughulikia migogoro na Mama Samia naye? Sasa si tumepiga Azimio leo asubuhi si ndiyo?

MBUNGE FULANI: Yes!

MHE. HALIMA J. MDEE: Tukamsifu Mama anaupiga mwingi si ndiyo? Sasa kuupiga mwingi siyo kwa mabarabara, kuupiga mwingi ni kwa agenda zinazogusa Watanzania. Wafugaji walio wengi, wakulima walio wengi, wachimbaji madini walio wengi na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ninaomba sana nimelizungumza hili kwa sababu it pains, watu wanaumia halafu vijisenti vidogo vidogo tunashindwa kuvitoa ili kusaidia hili tatizo litatuliwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho ni suala la mradi wa Kawe. Kwanza nitambue baada ya kuhangaika sana hatimaye project ya National Housing 7111, 7112 ya Shilingi Bilioni 45 inaenda kufanyakazi. Kwa hiyo, niwapongeze Wizara japokuwa tulizembea nchi ikapata hasara Bilioni 100, tusifanye uzembe wa namna hii tunaliumiza Taifa kwa kuchelewa kufanya maamuzi makini kwa wakati makini na kwa dhamira njema kusaidia nchi.

Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana. (Makofi)