Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Mwanakhamis Kassim Said

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi kunipa nafasi hii kuweza kuchangia jioni hii ya leo. Mimi nichukue nafasi hii kwanza kumuombea Mama yangu Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayofanya nchi hii Mwenyezi Mungu ampe nguvu ampe afya, ampe uzima lakini ampe uvumilivu ampe na Subira, Mwenyezi Mungu tunasema Alhamdulillah basi Mwenyezi Mungu anakuwezesha kwa mambo mengi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite moja kwa moja nimpongee Mheshimiwa Waziri wa Ardhi na Naibu Waziri na Katibu Mkuu na Viongozi wa Wizara hii kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuitumikia nchi yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nijikite moja kwa moja kwenye Wizara hii ya Ardhi, wenzetu hawa Wizara ya Ardhi wanafanya mambo makubwa, mimi ni Mjumbe wa Kamati hii tumezunguka maeneo mengi wanafanya kazi kubwa sana, migogoro hii itaendelea kuwepo na itakuwa ipo madhari sisi binadamu bado tupo kwenye dunia hii. Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi imeandikwa kuwa ardhi itapimwa nchi nzima na sisi tunatarajia ni hivyo kwa sababu nia ipo na sababu ipo ya kupimwa ardhi ya nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumza migogoro, migogoro ni binadamu, sisi ndiyo tunayoitengeneza lakini na wale wanaosimamia kwenye kitengo hiki cha ardhi, pale wamefanya neno lililokuwa zuri basi tusema Alhamdulillah tuwashukuru tuwapongeze na Mama yangu, Dada yangu wanafanya kazi kubwa sana. Kwa kweli ardhi ilikuwa mahtuti iko ICU lakini leo ardhi inazungumzika, migogoro mingi imetatuliwa, mambo mengi yamefanywa, kwa hivyo tuseme tu tuwaombee wenzetu waendelee na kazi hii kazi hii ni kubwa, kazi hii siyo ya mtu mmoja ni yetu sote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jukumu letu sote Wabunge kusimamia ardhi na kusimamia wananchi wetu tusiipe nguvu migogoro, kwa sababu tunalaumu migogoro lakini kuna migogoro mingine inatengenezwa, na watengenezaji ni wanasiasa. Hapa tunapigia kelele lakini mimi ni Mjumbe wa Kamati tumezunguka sana, hatujamaliza lakini tulikoenda kote ni kuzuri watu wanapewa hati zao wanapokea kina mama, baba, vijana, kwa kweli wenzetu wanafanya kazi kubwa, mimi nasema Alhamdulillah Mwenyezi Munge awawezeshe waendelee kuwatumikia watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukizungumzia ardhi usimsahau Mheshimiwa Lukuvi. Mheshimiwa Lukuvi alifanya kazi kubwa sana ya nchi hii, alipewa Wizara ya Ardhi iko mbovu, huwezi kufanya ziara kamati ikienda kwenye sehemu ya ardhi kama utapokewa, ilikuwa ni matatizo makubwa lakini Alhamdulillah unapokwenda wananchi wanakuelewa wanaweka vikao wenyewe wanakuita mnazungumza mnapaga wanataka kupimiwa ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mie niombe Serikali na Waziri wa Fedha yupo Wizara ya Ardhi hii iongezewe pesa, pesa ni ndogo wanayopewa hata tukiwalalamikia waje watupimie au watusikilize watu wanataka kupimiwa ardhi pesa ni ndogo wanayotengewa, kwa hiyo mimi nilikuwa naomba Serikali lazima isimamie ardhi. Ardhi ni kila kitu na wananchi sasa hivi ni waelewa wanajua kila kitu, kwa sababu ardhi ndio kila kitu, kilimo ardhi, ukienda kwenye maji ardhi, ukienda sehemu zote lazima tuwe na ardhi nzuri safi iliyokuwa haina migogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Lukuvi alifanya mambo makubwa sana, sisi tumekwenda Kigamboni tulipokewa kwa mapanga na kama Mbunge wa Kigamboni yupo ananisikia, alitupigia simu tulifika kwenye Pantoni hatukushuka lakini wananchi walituzonga, lakini leo nenda Kigamboni utapokewa na ngoma utapigiwa kwa sababu ardhi imepimwana ambayo haijapimwa lakini itapimwa kwa sababu ni ilani ya Chama cha Mapinduzi na Waziri wetu ni wa Chama cha Mapinduzi na Naibu Waziri ni wa Chama cha Mapinduzi, kwa hiyo ni lazima ardhi itapimwa lakini tunaomba pesa Wizara ya Ardhi iongezwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite moja kwa moja kwenye National House, National House pia walifanya kazi nzuri. Ndugu yangu Mchechu alifanya mambo makubwa sana, huyu kijana alifanya mambo makubwa sana, kwa hivyo tumpongeze na tumuombee kwa Mwenyezi Mungu amerudi pale pana viporo tele alivyovianzisha sasa aviendeleze viporo vile lakini nimuombe Mheshimiwa Mchechu arudi Kigamboni, tulisema tutaupanga Mji uwe wa Kisasa kwa hivyo warudi pale waende wakaupange Mji wa kisasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri nisema naunga mkono hoja. (Makofi)