Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi. Kwanza kabisa nampongeza Mheshimiwa Rais kwa Tuzo ambayo Azimio la Bunge leo limepitisha. Nilifurahi sana kilichoandikwa kwenye tuzo ile, nanukuu: “The First Female President in East Africa Region, the only Female President in Africa for 2022, for your dedicated services that proves the women ability.” Mheshimiwa Waziri nikupongeze sana, tunataka tuone the women ability kwenye Wizara hii ya Ardhi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza pia Naibu Waziri, Wakili Msomi Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete. Combination of the women ability na Wakili, tunatarajia kwa kweli Wizara hii migogoro tunayoisikia kutoka kila mahali itapata majawabu. Kwa kweli niwatie moyo, haya mnayoyasikia kutoka huku, tunawaambia tu kwamba kazi iliyo mbele ni kubwa zaidi, but we will support you. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza pia Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Dkt. Allan Kijazi, very humble na uzuri ametoka Wizara ya Maliasili na Utalii, na anajua kelele nyingi zilikuwa zinatoka Wizara ya Maliasili na Utalii kwa sababu ya migogoro mingi ambayo ipo. Kwa hiyo, sasa hii timu, with that experience, kwa kweli tunatarajia mengi zaidi na migogoro hii itapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ilileta mapendekezo ya sheria tumepitisha mwaka jana, na kwa kweli wameleta maboresho makubwa sana kwenye sheria ile ya migogoro kwa kupunguza nguvu za Mabaraza ya Kata ili waweze tu kusuluhisha tu migogoro kwa sababu ilionekana walikuwa wanafanya ambavyo sivyo kisheria. Wao wabaki kusuluhisha halafu Mahakama zile za ardhi zenye watu ambao wana uelewa wa kisheria wafanye kazi nzuri zaidi. Kwa hiyo, natarajia hayo yatakuwa ni mapinduzi makubwa yenye kuleta harmony kwenye migogoro ambayo ipo sasa. Pia walibadilisha sheria na Bunge hili lilipitisha sheria kuruhusu Kiswahili kitumike. Hii itasaidia wananchi kufuatilia hukumu zao kwa Lugha nyepesi kabisa wanayoifahamu. Big up. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa lililozungumzwa hapa ni la migogoro. Ni kweli tuna migogoro mingi sana vijiji kwa vijiji, mipaka ya vijiji na Hifadhi za Taifa, wakati mwingine mikoa kwa mikoa kubwa sana, na tunashukuru sana. Ni kweli waliompongeza Mheshimiwa Lukuvi, kwa kweli tunatambua sana kazi yake aliyoifanya kubwa. Nakumbuka walikuja Mawaziri nane kule kwangu kule Kiteto Kijiji cha Arkyush kwa mgogoro ambao umedumu kwa miaka 20 kwa Pori la Mkungunero na vijiji. Kwa kweli inashangaza sana kwa sababu GN iko clear sana na Mheshimiwa Rais Hayati Mkapa alisaini mwaka 1996, lakini eti ramani ambayo inachorwa na Maliasili na Utalii ndiyo inasema ile ramani ina-extend kwenda Kiteto. It is a bit funny kwamba ramani eti GN iliyosainiwa na Rais zinapishana, lakini hii yote inatokea kwa sababu wale walichora ramani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ardhi msiruhusu mtu yeyote nchi achore ramani yake. Sheria iko clear sana, ninyi ndio custodian wa ardhi nchi hii. Mkishatutawanyishia mkasema hii ni ya Kijiji, hii ni ya Hifadhi, hii ni general land, ninyi mnabaki kusimamia. Mwenye shida yoyote anakuja kwenu. Siyo mtu anataka ardhi ya Kijiji, anachora ramani mwenyewe, anapeleka GN mwenyewe, haiwezekani. Msiruhusu tena. Najua migogoro mingi mnayopata ninyi inasababishwa na watu wengine. Kwa hiyo, mkisimama firm ninyi ndiyo custodian wa ardhi nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma Kifungu cha 181 cha Sheria ya Ardhi, inasema, leo tukitunga sheria nyingi nyingi kidogo, ikatokea mgongano wa sheria hizi, on lands’ matter Sheria ya Ardhi takes precedent on lands’ matter. Kwa hiyo, wakati mwingine sijui migogoro inatokea wapi? Inatosha kwa Waziri wa Ardhi kusema Hapana. Akishasema hapana definition inayotokana na Sheria ya Ardhi ndiyo inakwenda hivyo. Siyo Sheria ya Wanyamapori. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mwingine kijiji kipo miaka 20, Wenyeviti wamechaguliwa miaka 20, TAMISEMI inatambua, ina CVL lakini kuna mabingwa wengine wanakuja wanatengeneza ramani wanaingiza kwenye vijiji halafu inaanza migogoro. Nadhani migogoro hiyo muihamishe kutoka field ije kwenye Ofisi zetu hapa. Waje kwenu mkae TAMISEMI, Ardhi na Maliasili. Kaeni mnyongane Ofisini huku, but don’t bring the confusion kwa wananchi, kwa sababu hakuna mwananchi anachora CVL ni Taasisi za Serikali wala hakuna Kijiji kinachojiandikisha chenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, this time Mheshimiwa Attorney General ambaye namheshimu sana, I think is the only man ambaye amekuwa DPP akaenda Judiciary na sasa Attorney General. Sometimes migogoro inazuka, unakwenda Mahakamani, unashindwa ku-enforce eti kwa sababu unakuta ng’ombe, bingwa mwingine kauza na kesi inaendelea Mahakamani, tusikubali. Jana Mheshimiwa Mbunge wa Morogoro Kusini aliongea vizuri sana na naomba niwashawishi Wabunge hapa; hapa tumeletwa na wavuvi, wakulima na wafugaji. Ikija issue inayomgusa mkulima, mfugaji na wavuvi tusimame, wala hakuna Mbunge hapa ambaye ana wafugaji peke yake kwenye Jimbo lake, wala hakuna mkulima ambaye eti ana wakulima peke yake kwenye Jimbo lake. Sisi wote ni viongozi tusimamie migogoro hii bila kuvuta upande wowote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nawapongeza wananchi wangu wa Kiteto. Kiteto imetulia sasa, lakini bado kuna vitu kidogo kidogo hivi; mara mfugaji ameingiza ng’ombe shambani, unaambiwa kuna mkulima ameingia kwenye maeneo ya kilimo. Hiyo ipo kidogo kidogo, lakini to be exact, imetulia. Nawapongeza sana wananchi wangu wa Kiteto. Nami nawaambia kupitia Bunge hili, mimi sina mtoto wa mgongoni na wa kifuani; wakulima, wafugaji wote wanaoishi Kiteto ni wa kwangu. Wote nawaomba mwendelee kutulia hivyo hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ardhi, Mifugo na Wanyamapori, tulikuwa tunaongea hapa na yule Mbunge wa Morogoro Kusini, migogoro hii siyo ya kwenu peke yenu. Mkitengeneza maeneo hotspots yenye migogoro, mkatengeneza ma-champion Wabunge hapa Bungeni, tutasaidiana tuende tuelimishe wananchi wetu na migogoro hii itapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesoma ripoti ya Kamati hapa na kwa kweli Wizara imekuja na very ambitious plan kwa kweli nzuri sana, wanataka kupima asilimia 50 ya Kijiji, lakini Tume ile ya Matumizi Bora ya Ardhi wana upungufu wa Shilingi bilioni tisa. Kwa kweli tuwasaidieni. Mheshimiwa Sillo rafiki yangu Kamati ya Bajeti hebu mtafute Shilingi bilioni 10 muwezeshe hii Tume ya Matumizi Bora ya Ardhi ili Vijiji vipimwe. Vijiji vikipimwa, migogoro itapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwashawishi wote kwa kweli tupitishe bajeti hii ya Wizara hii wakafanye haya yote ili mwakani tukutane hapa wakati tuna furaha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nakushukuru sana. (Makofi)