Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuchangia bajeti ya Wizara ya Ardhi. Kipekee kabisa nimpongezee Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete na kipekee zaidi Mheshimiwa Rais kwa kupata tuzo kwa sababu nchi za nje zimetambua mchango mkubwa wa maendeleo anayowaletea Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara hizi tatu, TAMISEMI, Maliasili na Ardhi ndiyo chanzo cha migogoro kwa wananchi, kwa sababu hizi Wizara hazikai pamoja zikaja na muelekeo mmoja wa namna ya kutatua migogoro kwa wananchi. Kila Wizara inafanya kazi kivyake, kuanzia sasa hivi wanatakiwa wakae pamoja, waje na jibu moja namna ya kutatua migogoro kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo langu lina kata 11, kata sita zote sehemu ambayo ni salama haina migogoro ni Makao Makuu ya Kata; Vijiji vyote vinavyozunguka kwenye hizi kata sita vyote vina migogoro ya ardhi. Ukigeuka huku kuna ranchi, ukigeuka huku Hifadhi ya Lwafi, hii Hifadhi ya Lwafi wananchi wa Jimbo la Nkasi Kusini pamoja na Rukwa ni wakulima. Lakini hizi hifadhi wananchi wameongezeka, lakini sehemu ya kulima wanapata tatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nakuomba Mheshimiwa Ridhiwan - Naibu Waziri, baada ya kikao cha Bunge break ya kwanza njoo Rukwa kuna migogoro mikubwa sana ya ardhi, umasikini wa Mkoa wa Rukwa unachangiwa na migogoro ya ardhi. Njoo utataue migogoro ya ardhi Mkoa wa Rukwa ili wananchi waweze kufanya kazi, waweze kulima kwa amani kwa sababu ni wachapakazi ili wanakwamishwa na migogoro ya ardhi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano Jimbo langu la Nkasi Kusini, vijiji vya Mkukwe, Kwamachindo, Mkata, China, King’ombe, Nundwe, Yasimba, Tundu, Tolesha, Izinga, Mwinza, Yela, Kwemanchindo hawa wote wako ndani ya hifadhi, akigeuka huku ni Ranchi ya Mkalambo, akigeuka huku Ranchi ya Nkundi; kwa mfano Ranchi ya Nkundi ni shamba la mwekezaji. Kijiji cha Nkundi hakuna hata eneo la kuweza kujenga shule, ofisi, mambo ya kijamii eneo hakuna.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe Mheshimiwa Waziri njoo utupatie Kijiji cha Nkundi eneo la kujenga shule kwa sababu hili shamba la Nkundi linapakana na kijiji. Wanakijiji wanahitaji maeneo ya shule, ofisi na mambo mengine ya kijamii pamoja na zahanati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vinavyozunguka mfano Kalambo, Kalambo Ranch; Kijiji cha Sintali Komanchindo hawana eneo la kulima linapakana na hifadhi ya Lwasi, mwiba mkubwa zaidi Mkoa wa Rukwa ni shamba la Efatha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Deus Sangu ameongea jana, hii ni ajenda ya Wabunge wote wa Mkoa wa Rukwa huyu mwekezaji amekuja sio kuwekeza, ni udalali, mashamba yanakodishwa, wananchi hawana maeneo la kulima, wakilima anaenda kupitisha trekta heka 100, heka 50 anavuruga mashamba ya wananchi, wananchi wanakamatwa akina mama wakipelekwa mahabusu kesi inaisha mahakamani hawa na lolote wanarudishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Rukwa hasa shamba la Efatha ni mwiba, Kijiji cha Sikaulu wananchi wamekuja kufika hapa sisi Wabunge tumeanza kuhangaika kutatua migogoro ya shamba la Efatha. Mheshimiwa Waziri wewe ni mcha Mungu, Mheshimiwa Ridhiwani tukimaliza hapa njoo anza na Efatha. Unapokuja kuhitimisha uje useme mgogoro wa Efatha unaisha lini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Rukwa ni wakulima, wanafanya kazi nzuri zaidi, wanahamia shambani kwenda kuweka makambi ili apate muda wa kulima, Wizara inaenda Maliasili wanachomea watu, wanafukuzwa wanaharibiwa mashamba yao hii sio haki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Wizara break ya kwanza njoo Rukwa uje utatue migogoro ya ardhi Rukwa inachangiwa umaskini kwa sababu Wizara hii haijaitendea haki Mkoa wa Rukwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naunga mkono hoja. (Makofi)