Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kwenye Wizara hii ya Ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote kwanza nitumie nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kufanya uteuzi mzuri wa dada yangu Dkt. Angeline Mabula kuwa Waziri mwenye dhamana na Wizara hii ya Ardhi na Makazi, lakini pamoja na hilo pia kwa ndugu yangu rafiki yangu, Mheshimiwa Naibu Waziri, Ridhiwani Kikwete kuwa ni msaidizi wa Mheshimiwa Mabula. Lakini nitambue kazi nzuri inayofanya na Wizara, kwa maana ya watendaji wao wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo nitasema kidogo tu kwenye eneo ambalo mara nyingi nikipata nafasi nalisemea kama kuikumbusha Wizara na eneo lenyewe ni jambo la urasimishaji. Mjumbe mmoja kule upande wa pili alinyanyuka akaweka kibwagizo tu kwamba wananchi wanatakiwa waelewe sana nini maana ya urasimishaji na akatoa mfano yeye anatoka Tabora lakini akasema hasa kule Dar es Salaam, mimi nikapiga makofi hapa mawili matatu nilitaka kumwambia ni kweli tunatamani kujua maana ya urasimishaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi hiki ni kidonda kisichopona, hili kwetu ni tatizo, mwaka jana nilisema hapa, nilisema tukatofautina tofautiana na Mheshimiwa Waziri akiwa Naibu Waziri, moja kwenye swali la msingi lakini baadaye hata wakati nachangia kwenye fungu hili. Hoja yetu pale tunajua na huku imesemwa kwenye ukurasa wa 43 urasimishaji kwa ujumla katika jukumu la kupanga, kupima na kumilikisha ardhi, sehemu kubwa ni jambo la mamlaka zetu za Miji na Halmashauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tunatambua kule Dar es Salaam jambo hili wamepewa makampuni kufanya na Mamlaka za Miji haya makampuni tunaanzia hapa, yameletwa na kupewa ithibati kwa kuwa scanned na Wizara yaani wananchi wetu kule so tu wamepokea makampuni au walikaa wenyewe wakasema aje huyu au aje yule, Wizara mliangalia makampuni yale, lakini mwisho wa siku mkasema sasa nendeni mkaingie katika Halmashauri zenu za Miji na Halmashauri na Halmashauri za I mean katika miji yetu ili wafanyekazi na wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, imekuwa tatizo, mwaka jana nilisema wizi mkubwa, makampuni yametuibia, fedha nyingi tukatofautiana hapa, lakini mimi nakumbuka Naibu Waziri amekuja juzi tu, kabla ya kuwa waziri wakati mdogo tu kabla hajawa Waziri ameona, kwamba kama tumetofautiana figure, lakini zaidi ya bilioni nane aliziona kabisa kwamba iko shida sehemu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukweli nitumie nafasi hii nimpongeze sana Mheshimiwa Kheri Dennis James, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo nampongeza kwa sababu amechukuwa hatua za awali lakini amepata ushauri baada ya kutembelewa na Mheshimiwa Waziri kwamba tufike sehemu, yale makampuni baadhi yake wakasimamishwa, lakini bado hoja yangu fedha za wananchi ziko wapi, mwaka jana nikasema jicho la tatu lije, hata kama CAG nikawashauri mleteni ili ajue hela za wananchi ni kwa kiasi gani zimeibiwa hakuna.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mwaka jana tuliambiwa mradi huu wa miaka kumi unaenda kuisha mwezi Oktoba 2023; mwaka 2023 ni kesho kutwa sisi bado hela tumepoteza mabilioni ya hela, lakini dhima inasemwa humu, lakini dhima ya kupima, kupanga na kutoa hati, ni kuboresha maisha na uchumi wa wananchi sasa sisi tunafanya nini tunaendelea kuwa maskini hati hatuna, ardhi yenyewe tunakuwanazo kwa shida.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri kwa haraka; nimeona hapa wewe ni shahidi inazungumzwa miji shilingi bilioni 45.7 huku amesema kama bilioni hamsini hivi zinapelekwa kwenye Halmashauri 25, kwa ajili ya jambo hili hili la kupima kupanga na kumilikisha ardhi, wakati mwaka jana nilisema kila mwaka zinawekwa zinaenda huko, shilingi bilioni 50 wengine wanapewa kwa jambo lile Dar es Salaam inaachwa tena, kwa hiyo wananchi wanatoa wenyewe na wana hali mbaya na zinaibiwa na hatufanyi chochote.

Mheshimiwa Naibu Spika, mim niwaombe sana Mheshimiwa Waziri nataka nikushauri na katika hili naomba uniruhusu nimwomba na Waziri Mkuu aliingilie jambo hili na aje Kibamba kwenye Jimbo lile na Wilaya nzima ya Ubungo aone anatutatuaje, pelekeni chukuweni jukumu ile hela yote iliyopota fanyeni ninyi ndio imepotea kwenu kwa sababu mlileta ninyi yale makampuni. Wapelekeeni zile demand kwa ajili ya kulipia hati tu, ile ndio wadaiwe wale wananchi ambao wameibiwa zile fedha na yale makampuni mliyoyaleta ninyi huo ndio ushauri katika eneo hilo. Nafikiri nitakuwa nimeeleweka siku ya leo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili Mlonganzila pale miaka ya nyuma kidogo wananchi watakumbuka tumepeleka pale hospitali ya Mlonganzila kulikuwa wananchi wanaishi katika lile eneo zaidi wa wananchi 2500, eneo lile ambalo kuna Hospitali ya Mlonganzila, lakini mimi nishukuru sana Serikali zetu zote hizi ziliona hiyo sababu ikawalipa mali zao, iwe mazao na nyumba zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa sababu ya eneo hili baada ya tathimini kubwa ilionekana la Tanganyika Packers basi wakati ule namkumbuka alikuwa Angellah Kairuki alifika na wakakubaliana kama neno la Serikali kwamba tutawalipa kifuta machozi shilingi milioni mbili kwa kila ekari mwaka 2015/2016 mpaka leo, sijui ni kwa sababu tulikuwa tunaenda kwenye uchaguzi wa 2015 hakuna kilichofanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Mheshimiwa Waziri hili jambo mlikumbuke, muende kule wananchi kule wanalia mkalipe kile kifuta machozi mlichokiahidi cha shilingi milioni mbili kwa kila ekari. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, zaidi ya mwisho dogo juu ya kuboresha miji ya Dar es Salaam kama maendeleo katika maeneo ya Tandale nilishalisema wakati nachangia Waziri Mkuu, maeneo ya Manzese, maeneo ya Magomeni kama tulivyofanya Magomeni quarters tubadilishe uchumi wa Dar es salaam ili maisha ya watu yawe bora. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, naunga mkono hoja. (Makofi)