Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kuungana na viongozi wenzangu wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa majaliwa yake kwetu sote, kwani tunajivunia kwa jinsi alivyotuvusha kwenye majanga mbalimbali kwa mfano corona na majanga mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kwa niaba ya wananchi wote wa Jimbo la Mbulu Mjini kutoa pongezi nyingi sana kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wetu mpendwa kwa jinsi anavyoiongoza nchi yetu na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020 – 2025.

Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kuwapongeza Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mheshimiwa Waziri Mkuu, Waziri wa Wizara hii Mheshimiwa Naibu Waziri wa Wizara na Mheshimiwa Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii kwa jinsi mnavyoitendea haki Wizara hii; kwanza kutusikiliza sisi wawakilishi wa wananchi na kutatua tatizo la kuzuia ujenzi holela na kuleta kupanga, kupima na kumilikisha (KKK) kwa nchi nzima, hongereni sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna ya pekee naungana na viongozi wenzangu kutoa pole nyingi kwa familia zilizopata msiba ya kuwapoteza wapendwa wao kuanzia kwa viongozi wote, watendaji na Watanzania wote, Mwenyezi Mungu atujalie hali ya ustahimilivu katika kipindi hiki, sote kwa pamoja tunaziombea roho zao kwenye ufalme wa mbinguni usio na mwisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nitoe mchango wangu kupitia hotuba ya bajeti ya mwaka 2022/2023 ya Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nachukua nafasi hii kuipongeza sana Serikali yetu kwa kuleta mpango wa kupanga, kupima na kumilikisha ardhi katika Halmashauri zote nchini na kuonesha mafanikio makubwa sana kukabiliana na kuzuia ujenzi holela na kurasimisha ardhi kuwa na thamani kubwa na miji itakayopangika.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi kuna baadhi ya changamoto zinazozuia jitihada hizo zikiwemo upungufu mkubwa sana wa vitendea kazi, watumishi wa kada muhimu katika idara za Ardhi ngazi za Wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaiomba sana Serikali iwaajiri wataalam wa kada muhimu katika kufanikisha mpango huu muhimu sana kwenye bajeti ya mwaka huu. Tunashukuru sana Serikali kwa kuondoa baadhi ya maamuzi/hukumu katika Mabaraza ya Kata kwa kuwa baadhi ya walalamikaji na walalamikiwa kutokuridhika na maamuzi ya mabaraza ni muhimu sana Serikali kuwa na mfumo wa kuchunguza mabaraza yanayolalamikiwa hasa kwenye mashauri mengi yanayogusa Serikali za Vijiji, Halmashauri za Wilaya, taasisi za Serikali na watu binafsi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaipongeza sana Serikali kwa mpango wake wa kutumia timu ya Waheshimiwa Mawaziri na watendaji kufanya ziara ya kutatua migogoro nchi nzima. Kwa hiyo ni muhimu sana kabla ya timu hiyo kuondoka wakatoa nafasi kwa waheshimiwa Wabunge wa maeneo hayo kama wawakilisha wa wananchi ili kupata na kuelewa historia na chimbuko lenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ijitahidi kukusanya mapato yake ya ndani kwa 100% ili kufanikisha lengo lake kwa mwaka wa bajeti kwani kiwango cha 42% kilichokusanywa mwaka 2021/2022 ni ndogo vinginevyo kufanyike mapitio ya kina kwenye vyanzo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho siyo kwa umuhimu tunaiomba sana Serikali ijitahidi kutoa fedha zinazoombwa na Wizara hii ili kufanikisha malengo kwani kiwango cha 51% kwa fedha zilizotolewa na Serikali 2022/2023 ni ndogo sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa silimia mia moja na naomba kuwasilisha.