Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Angelina Mabula (Mb) na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Nampongeza pia Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete (Mb) na Naibu Waziri, Ndugu Allan Kijazi - Katibu Mkuu pamoja na Naibu wake Ndugu Nicodemus Mkapa kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina maombi yafuatayo; kwanza kumaliza mgogoro wa Lipalamba Game Reserve na Kijiji cha Mseto kilichopo kata ya Lipalamba; pili, Wilaya ya Nyasa ni changa sana kimapato. Tunaomba mkopo ili kupima maeneo ya fukwe yote na Mji wa Mbamba Bay ili usijengwe kiholela.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.