Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante na mimi nikushukuru kwa ajili ya kunipa nafasi hii, lakini pia na mimi nimshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuona umuhimu wa kuanzisha Wizara hii ya Maendeleo ya Jamii, lakini pia nimpongeze Waziri pamoja na wenzie wote kwa kazi kubwa ambayo wameanza kuifanya kwenye Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, mimi leo naomba niongelee watoto wa kiume; tangu uumbaji Mungu alivyoumba utaratibu kila kitu kina namna ya kuongezeka na katika baraka ambazo Mwenyezi Mungu alizitoa kwa viumbe alivyoviumba tukiwepo wanadamu alisema tukaongezeka, tukatiishe, tukazalishe na tukatawale, hivi ni vitu ambavyo Mwenyezi Mungu, lakini sasa tunakwenda kuongelea pale kwenye kuongezeka.

Mheshimiwa Spika, kuongezeka kwa wanadamu au mbegu ya wanadamu Mwenyezi Mungu ameiweka ndani ya mtoto wa kiume, hakuna namna utabisha hilo. Na hata katika wanyama mbegu yao ya kuongezeka ipo ndani ya yule mnyama wa kiume, kwenye samaki hivyo hivyo yaani kwenye viumbe vyote ni hivyo. Sasa watu wote wenye afya nzuri ya akili wanaitunza mbegu kuliko kituo chochote, mkulima yeyote mwenye busara anaitunza mbegu yake vizuri kuliko kitu chochote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na ndio maana mimi siwezi kuwa mshabiki wa kwamba mwanaume akifanya kosa ahasiwe kwa sababu mwisho Watanzania tutakosa mbegu na tukikosa mbegu tukaenda kuagiza kutoka nje sio Watanzania; na tukiitwa mbinguni kule tutaonekana Taifa letu liliisha siku nyingi sisi ni Taifa lingine. Sasa ninachotaka kusema, namna ambavyo tunaangalia watoto wetu wa kiume nchi hii sio sawa, naomba Mheshimiwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii alichukue ile ni mbegu, tukianza kwenye level ya familia tuangalie namna tunavyowalea watoto wetu wa kiume. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mbegu unajua inaweka kwenye kihenge inatunzwa vizuri isibunguliwe, lakini leo kwenye level ya familia ukiangalia mtoto wa kike ameweka karibu kabisa na chumba cha baba na mama ili hata akitoka usiku washtuke wamlinde, mtoto wa kiume amewekewa chumba banda la uani huko, arudi hakurudi hakuna anayejua. Leo hii kwenye familia tunasema kwamba hawa ndio vichwa vya familia, lakini ukiangalia namna tunavyowalea sio kuja kuwa vichwa, ndio maana kunatokea mgongano sasa hivi, huwezi kutegemea kumlea mfalme halafu ukamlea kilezilezi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hii tuangalie wengi hapa tunaweza tukawa tunaangalia kwenye Azam pale sinema ya Ertugul angalia Ertugul jinsi alivyo m-raise Ottoman, alivyompeleka vitani, alivyomsimulia kwamba wewe ni mfalme, alivyomfundisha na kumpa mbinu, alivyomlisha, alivyompeleka shule na kumpa maarifa ya kwamba yeye ni mfalme, lakini sivyo tunavyowalea watoto wetu wa kiume. Leo hii tunaanza kuwapa sifa za ufalme kabla hajafika kwenye kuwa mfalme, mtoto wa kiume anapendelewa, anapewa vitu hata akiumia tu wakati mwingine anahitaji faraja alie, amwambie mama mimi nimefanyiwa kitu kibaya leo watoto wetu wanalawitiwa kwenye majumba kwa sababu ameshaambiwa mtoto wa kiume halii lii, mtoto wa kiume hasemi semi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo anasindwa hata kujieleza tatizo lake, leo hii ukienda mitaani waliojaa ni watoto wa kiume, sio wa kike, wameachwa, leo hii tukienda kwenye elimu tukianza kuweka kipaumbele hapa tunaweka kipaumbele cha kujenga hostels tunajenga za wanawake sio za watoto wa kiume. Sisi tunaangalia equality hatuangalii equity, sasa huyu unayetegemea aje kuwa kichwa leo hii twende kwenye style tunavyowaozesha watoto wetu, watoto wa kike wanaitwa wanapewa kitchen party wanapewa mafunzo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa MzungumzajI

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ninachotaka kusema lazima sasa tubadilishe style ya kuangaia watoto wetu wa kiume na kuwapa haki sawa kwenye elimu, kwenye matibabu kwenye mafunzo kwenye kila kitu ili tuanze kuwa na kichwa kilichoenda shule, kama tunajua ile ndio mbegu yetu lazima tuitunze kwa ubora wote bila kuangalia kwamba …

SPIKA: Haya ahsante sana.

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: … hawa ni watu wa aina gani, ahsante naunga mkono hoja. (Makofi)