Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi na mimi kuchangia. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuianzisha hii Wizara ya Maendeleo ya Jamii kwani ilipokuwa pamoja na Afya niliona kama ilikuwa inamezwa.

Mheshimiwa Spika, tena niwapongeze sana wanawake wote wa Tanzania, kwa kweli wanawake sasa hivi hakuna mwanamke aliyelala. Hata ninyi wanaume mliyo humu ndani mnajua wake zenu wanafanya kazi, hakuna mwanamke aliyelala, kwa hiyo nawapongeza sana. Na wanawake wengi wamejitolea sana kufanya usindikaji, kufanya biashara mbalimbali, wanafanya kazi kweli, tatizo nilikuwa naomba Wizara waone jinsi ya kuwapatia mafunzo ya biashara wanawake kwa sababu wengi wanaanzisha biashara bila ya kupata mafunzo. Wapate mafunzo ya biashara pamoja na ujasiriamali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikiendelea hapo hapo nimekazia kuwa wapatiwe mafunzo ya biashara pamoja na ujasiriamali. Wanawake wamejitoa sana, hakuna mwanamke aliyelala sasa hivi.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo ninasema ni asilimia nne kwa akinamama. Kwa kweli hawa akinamama wanarudisha mikopo yao vizuri sana na wanaitumia, lakini wanawake ukweli wamenituma wanasema kuwa hii asilimia nne haitoshi. Kwa hiyo, tuangalie pamoja na kushirikiana na Wizara zingine jinsi ya kuona tufanyeje ili ionekane hizi asilimia nne ambao wanapewa hawa akina mama, pamoja na vijana, pamoja na makundi ya watu wenye ulemavu ionekane kuwa kweli inafanya kitu ambacho kinaonekana kweli kweli kuwa ni kitu chenyewe.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni kwenye usindikaji; akinamama ambao wamejikita sana ni masoko waweze kutafutiwa masoko na waweze kuonyeshwa kuwa wafanye vitu ya vyakula ambacho kina quality kweli. Wakati mwingine vyakula havina quality unakuta kuwa TBS inawababaisha, kwa hiyo tuangalie tuweze kuwasaidia hawa akinamama.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine na mimi nawaunga mkono akinamama wote waliongelea kuhusu ukatili wa akinamama pamoja na watoto. Unaona kwa kweli ni mambo haya wanafanya kwa kweli, tunaomba wajirudi akina baba kuacha kufanya ukatili kwa watoto wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ninaloongelea ni watoto wa mitaani; tutaongelea watoto wa mitaani mpaka lini na yenyewe tuweke mtazamo jinsi ya kukatiza kuachana na kuongelea mambo ya watoto wa mitaani. Wizara pamoja na Afisa Maendeleo tukiwa pamoja na Ustawi wa Jamii tuone jinsi ya kuwaangalia hawa watoto waache kwenda kwenye mambo ya mitaani.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo halijaongelewa humu ni jukwaa la akinamama; majukwaa ya akinamama namshukuru Mheshimiwa Rais Samia ameanzisha majukwaa ya akinamama tangu alipokuwa Makamu wa Rais. Lakini mpaka sasa hivi haya majukwaa ya akinamama hawajui yanafanya nini, wapo tu, hawana uwezeshwaji, wanaendelea tu. Kwa hiyo, naomba sana wangepewa Mwongozo wangeliweza kufanya vizuri sana.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo naomba kuliongelea ni vituo vya wazee; nilitembelea vituo vya wazee vya Morogoro, Kituo cha Fungafunga pamoja Chasi. Unakuta kuwa vituo vya wazee wanamuomba Mheshimiwa Waziri na Naibu awatembelee, hawajawatembelea kwa sababu kuna matatizo mengi, lakini viongozi wengine tumekwenda ndiyo sababu tunayachangia. Unakuta hao wazee wanaishukuru kwanza Serikali inawapatia chakula, ila kwa chakula wanapongeza. Lakini kuna tatizo unakuta hawa wazee majengo yao ni mabovu, kwa hiyo nilikuwa naomba haya majengo yaweze kukarabatiwa.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine wazee hao wengine siyo wazee sana kwa sababu kuna na vijana ambao wameumwa ukoma, hawana vidole, wamekatika vidole na nini nao wako humohumo. Wanaomba Kituo cha Fungafunga waweze kupatiwa uzio kwa sababu wazee wanatoroka wanakwenda mjini.

Jambo lingine wanashukuru kuna ma-nurse, lakini kuna tatizo moja wakipata magonjwa dawa hazitoshi, kwa hiyo wanaomba wapatiwe dawa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo naongelea hapohapo ni maji; wana tatizo la maji naongelea Fungafunga ya Morogoro, kwa hiyo ushauri wangu waweze kupewa maji kusudi na na wenyewe waweze kutumika vizuri.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni watumishi; nikija kwenye watumishi, kuna watumishi wa Ustawi wa Jamii ambao inabidi wa wasaidie. Watumishi ni wachache kiasi wazee wengine hawajiwezi kabisa. Kwa hiyo, naomba muwaongezee watumishi. Hapo hapo kuna watumishi wengine wamekaa muda mrefu kwenye ngazi hiyo hiyo kuanzia mwaka 1999 hajapandishwa cheo chochote, yuko palepale, kwa hiyo, naomba muwaangalie na wenyewe waweze kuonwa kuwa wanafanyiwa mambo mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni kuhusu uhaba wa watumishi kwa ujumla na wajibu wao, maendeleo ya jamii ni watu wazuri na inabidi waweze kufanya kazi zao vizuri, waweze na wenyewe kupewa vitenda kazi kama Wizara zingine walivyopewa vitendea kazi kama pikipiki na nini. Kwa sababu masuala yote kwa Afisa Maendeleo ya Jamii ambaye anajijua masuala yote ya lishe yako kwako, masuala yote ya ujenzi wa vyoo yako kwake, masuala yote ya nini kusudi waweze kufanya kazi zao vizuri naomba Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii waweze kuangaliwa kwa vitendea kazi.

Mheshimiwa Spika, baada ya hapo nakushukuru kwa kunipatia nafasi. Kwa hayo niliyoyaongea, naunga mkono hoja. (Makofi)