Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Hon. Martha Nehemia Gwau

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

MHE. MARTHA N. GWAU: Mheshimiwa Spika, naomba nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na watendaji wote wa Wizara.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la ukatili kwa wadada wa majumbani ambao wamekuwa wakisaidia familia nyingi majumbani maarufu kama house girl; ni muhimu kuweka mkazo na kutoa elimu kwa jamii hususani kwa familia ambazo zinawachukulia wadada wa kazi kama watumwa na kuwatumikisha kinyume na utaratibu na maelewano. Mambo kadhaa ambayo wanapitia na kuwa yanahitaji kuangaliwa kwa ukaribu ni kama ifuatavyo; kwanza ni mishahara yao ilipwe kwa wakati na kiwango kiwe elekezi ili kusaidia wadada wa majumbani wapate haki zao; pili muda wa ufanyaji kazi na kupata hata siku moja ya mapumziko tofauti na sasa kuna baadhi ya familia wanawafanyisha kazi siku saba za wiki na bila mapumziko.

Mheshimiwa Spika, ni vyema Maafisa Maendeleo ya Jamii wakawaelemisha wadada wa majumbani kuhusu haki zao za msingi na ni wapi wakaripoti endapo watapata kunyanyaswa na waajiri wao na hasa suala la ukatili kwa kutaka kulazimishwa na baba tendo la ndoa kwa madai asipokubali atafukuzwa kazi.

Mheshimiwa Spika, nashukuru na naomba kuwasilisha.