Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, naungana na Watanzania wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa baraka kwa kuijalia nchi yetu amani, utulivu, mshikamano, ustawi wa jamii na kutuepusha na majanga mbalimbali yanayotokea mara kwa kote duniani.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kwa niaba ya wananchi wote wa Jimbo la Mbulu Mjini kutoa pongezi nyingi sana kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan - Rais wetu mpendwa kwa jinsi anavyoiongoza nchi yetu na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020 – 2025.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuwapongeza Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mheshimiwa Waziri Mkuu, Waziri wa Wizara hii, Naibu Waziri wa Wizara, Mheshimiwa Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii kwa jinsi mnavyoitendea haki Wizara hii kwanza kwa kutusikiliza sisi wawakilishi wa wananchi na kutatua changamoto mbalimbali tunazowasilisha kwenu, hongereni sana na Mungu awabariki.

Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee naungana na viongozi wenzangu kutoa pole nyingi kwa familia zilizopata misiba mbalimbali ya kuwapoteza wapendwa wao kuanzia kwa viongozi wote, watendaji na Watanzania wote Mwenyezi Mungu atujalie hali ya ustahimilivu katika kipindi hiki, sote kwa pamoja tunaziombea roho zao kwenye ufalme wa mbinguni usio na mwisho.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba kutoa mchango wangu kupitia mapendekezo ya hotuba ya Wizara hii na taarifa ya Kamati yetu ya Bunge; kwanza tunaipongeza Serikali yetu kwa kutoa fedha za ndani kwa ajili mipango ya maendeleo. Hata hivyo kwa kuwa Wizara hii mpya tunaiomba sana Serikali iongeze bajeti ya Wizara hii kwa kuwa ina mahitaji makubwa ya miundombinu, watumishi na vitendea kazi mbalimbali na kuendelea kutumia utashi wa kushawishi kupata fedha za nje kwa wadau.

Pili, kwa kuwa Wizara imeundwa kuna umuhimu mkubwa sana kufanya mapitio ya sheria zilizoko na mpya ili kusimamia na kuwezesha utendaji wa Wizara yetu kukabiliana na masuala mbalimbali kama vile wingi wa watoto wa mitaani na ndoa zinazotelekezwa na haki za mirathi na wajane.

Mheshimiwa Spika, tatu, Serikali iwaelekeze asasi za kiraia wapitishe mipango kazi yao kwenye vikao vya Mabaraza ya Madiwani, DCC na RCC kwa ajili ya kupata vipaumbele na kufanikisha mahitaji muhimu na mtambuka katika maeneo hayo.

Aidha, Wizara iandae mafunzo kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii kwa ngazi za Kata na Wilaya katika ratiba zake kila mwaka. Pia Serikali iangalie uanzishwaji wa Mabaraza ya Wazee kwa ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na Vijiji kurahisisha uratibu wa matatizo na changamoto mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, naunga hoja mkono asilimoa mia moja na naomba kuwasilisha.