Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Hon. Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, naomba Wizara iangalie na kufuatilia ili kulinda afya ya watoto wadogo wanaokwenda kwenye vituo vya kulelea watoto wadogo. Wapo baadhi ya wamiliki wa vituo hivyo ambao wamepata vibali isivyo halali kwani nimeshudia watoto wakirundikwa kwenye vyumba visivyokidhi haja kiafya wakati wa mchana wanaposubiri wazazi kuwafuata. Wanarundikwa kwenye vigodoro, wanalazwa kama samaki. Fuatilieni vituo hivyo hususani mkoa wa Dar es Salaam, hali si rafiki.

Mheshimiwa Spika, watoto hawa wengi ni kati ya mwaka mmoja hadi miaka minne, lakini cha kushangaza vituo hivyo vinachanganywa na watoto wa umri wa miaka mitano hadi sita wanaotakiwa wawe pre-school. Matokeo yake ni watoto wadogo wanaweza kulawitiwa na hawa watoto wenye umri usiotakiwa kuwa kwenye hivi vituo vya kulelea watoto. Tunaomba Maafisa Ustawi wa Wilaya wafuatilie na kukagua kwa kushtukiza vituo hivi.