Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, napenda kuwapongeza Mheshimiwa Dkt. Dorothy Gwajima (Mb), Waziri wa Maendeleo ya JamiII, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum; na pongezi kwa Naibu Waziri Mheshimiwa Mwanaidi Ali Khamis (Mb). Pia nampongeza Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu pamoja na watendaji wote wa Wizara.

Mheshimiwa Spika, kuhusu 10% inayotolewa na Halmashauri kwa ajili ya mkopo, nashauri ipatikane system maalum itakayohusika kusimamia vizuri ukopeshaji na ukusanyaji wa madeni kama ilivyo kwa mabenki. Pia vituo vya ushauri nasaha hakuna. Serikali ifungue dirisha maalum either kwenye vituo vya afya au ofisi za kata ili kusaidiwa. Familia nyingi zina changamoto za kifamilia, zinaumwa lakini hazina pa kukimbilia (counselling centres).

Mheshimiwa Spika, uhamasishaji wa maendeleo ya jamii upewe mwongozo maalum na wafanye mikutano ya hamasaki mara kwa mara. Pia umeanza unyanyapaaji wa wazee hata kuwasemasema bila heshima.