Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Ahmed Yahya Abdulwakil

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. AHMED ABDUL WAKIL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya mtu wa kwanza kuchangia kwenye Wizara hii muhimu sana ambayo inatuunganisha na dunia ya kisasa. (Makofi)

Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuamka salama na kwa utulivu mkubwa katika Bunge letu na hapo hapo nikimshukuru Rais wa Tanzania Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa na ya gear kubwa aliyoanza kwenye Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza sana Mheshimiwa Waziri Balozi Libarata pamoja na mkongwe Balozi Mbarouk kwa kazi kubwa ya kumsaidia Rais katika diplomasia ya uchumi. Timu yako ya Wizara inafanyakazi kubwa sana kwenda na kasi ya mama katika kuweka diplomasia ya uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo kubwa ambalo nalipongeza kwamba dunia si kijiji au dunia ni Kijiji, mama amekifanya kijiji kiwe chini ya mikono yetu hivi sasa na hakuja na diplomasia ya kuzungumza tu, lakini amekuja na diplomasia ya uchumi ambayo uchumi ni kila kitu katika dunia. Kwa hiyo, uteuzi wa balozi alioufanya karibu nchi 45 na umekiri kwamba hivi karibuni amefungua Balozi mpya ya Indonesia imeleta faraja kubwa sana katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Balozi hizi tunaziona zinavyofanyakazi katika mitandao mbalimbali kama Italy, USA, China, Korea na Balozi nyingine nyinginezo zinakwenda moja kwa moja katika kutekeleza diplomasia ya uchumi.

Mimi nitazungumzia uchumi tu, kwa hiyo ipo haja na hoja kwamba Balozi hizi Mheshimiwa Waziri zije na mpango kazi ambao tutahakikisha sasa kwa mfano nchi ya Turkey ni mzalishaji wa chuma, mzalishaji wa bati, vifaa vya uvuvi na vifaa vya marine. Kwa hiyo, tujikite kutafuta fursa zile pale kwa nchi yetu kusudi tuweze kufaidika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukija na balozi nyingine kadhalika wakija na mpango kazi madhubuti tutakuwa tunajua focus gani tunaweza tukapata maendeleo na kufaidika katika nchi zetu. Kwa jumla mimi sina mengi sana ya kuzungumza nakushukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kwamba ipo haja na hoja Zanzibar tusiishie ukarabati wa Wizara, ipo haja sasa hivi kwa miaka hii karibu 60 ya Uhuru lijengwe jengo la kisasa, wageni wakija tuachane na vichochoro vidogo vidogo viliopo ili kusudi Zanzibar nayo kuwe kuna jengo walau lenye hadhi ya kibalozi, (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hayo machache ahsante sana na naunga hoja mia dhul mia ahsante sana. (Makofi)