Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuwa mchangiaji wa pili na kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uhai na pia na afya njema.

Napenda kumpongeza Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa Mulamula, Naibu wake Mheshimiwa Mbarouk kwa kazi nzuri ambazo amezifanya na kwa kuonyesha kwamba wamefanyakazi nzuri leo hii tunao mabalozi ndani ya nyumba hii ambao wamekuja kusikiliza bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje nafikiri kwa mara ya kwanza ukumbi umejaa mabalozi na wawakilishi wa konseli mbalimbali tunakushukuru sana na tunaomba muendelee na moyo huo wa ushirikiano kwa nchi za jirani zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia nimpongeze Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri aliyoifanya ya kuifungua nchi yetu ya Tanzania na kidhibiti cha mambo haya ni pamoja na Balozi ambazo ziko hapa leo, lakini pamoja na mambo ambayo Serikali ya Tanzania imeyapata kutokana na Mheshimiwa Rais kufungua nchi yetu. Tumeona matokeo mengi sana kwa ziara za Mheshimiwa Rais tumeona ushirikiano jinsi gani Mheshimiwa Rais anashirikiana na Marais wengine lakini pia tumeona ni jinsi gani anakwenda kutafuta pesa za kuweza kuleta kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi sisi kama Wabunge tunatakiwa tumpongeze Mheshimiwa Rais kwa kuifungua nchi yetu ya Tanzania, lakini pia tunampongeza kwa tuzo ambazo ameendelea kuzipata hususani tuzo ambayo ameipata hivi karibuni aliyopewa na Benki ya Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya pongezi hizo napenda sasa kutoa mchango wangu mbalimbali kuhusu Wizara ya Mambo ya Nje. Kwanza kabisa napenda nizungumzie suala la viwanja vilivyopo kwenye Balozi zetu. Katika ripoti ambayo ameisoma Mheshimiwa Waziri nimeifuatilia na nimeisikiliza na kuisoma ameeleza ni jinsi gani Serikali ya Tanzania imeweza kupoteza viwanja vyake ambavyo vipo nje ya nchi, hususani kile kiwanja cha Ethiopia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nazungumzia Ethiopia kwa sababu nafahamu Serikali ya Tanzania ilikuwa na kiwanja pale na niliishi pale kwa hiyo naelewa yale mazingira ya pale Ethiopia kiwanja hicho kilikuwepo siku nyingi tangu miaka ya 2000 lakini nafikiri hatukuweza kuwekea mkazo kukijenga. Hivyo basi niombe Serikali ya Tanzania lakini kupitia Wizara hii ya Mambo ya Nje zile mali ambazo zipo nje ya nchi, hususani viwanja Serikali ijitahidi kujenga yale majengo ili watumishi wanaofanya kazi nje ya nchi waweze kukaa kwenye hizo nyumba ni gharama sana Serikali kupanga nyumba nje ya nchi, lakini tukiwa na jengo letu tutaweza kuokoa fedha zile ambazo zinalipwa kwa ajili ya pango la nyumba za wafanyakazi wanaofanya kazi Wizara hiyo. Niombe basi katika bajeti inayokuja Serikali ijaribu kutoa fedha ili majengo hayo yajengwe, (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia niombe kutoa msisitizo kwa mabalozi ambao wanateuliwa na Mheshimiwa Rais wanapokuwa nje ya nchi yetu ya Tanzania, wao ndio wawakilishi wa Watanzania wote, lakini pia wao ndio wawakilishi wa Mheshimiwa Rais. Niwaombe wanapokuwa kule kwenye zile nchi za nje waweze kutumia nafasi yao kukuza hii diplomasia ya uchumi ambayo Mheshimiwa Rais anapambana nayo sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kumuachia Mheshimiwa Rais peke yake kwenda kuongea na wadau nje ya nchi wakati kuna Balozi zipo kule ni suala pia ambalo Balozi anatakiwa alifanye, Balozi ni mwakilishi pale kwenye nchi ile, lakini Balozi anauwezo wa kukutana na wadau mbalimbali Wachumi akakutana na wawekezaji. Kwa hiyo Balozi anapokuwa kule kwenye nchi za nje azingatie kukuza diplomasia ya uchumi ambao Mheshimiwa Rais ameianzisha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ambalo ningependa kuzungumzia ni suala la diaspora, katika suala la diaspora nilikuwa naomba Serikali ijaribu kuangalia ni jinsi gani itaweza kuwa-accommodate Watanzania ambao wanakaa nje ya nchi. Mara ya mwisho niliweza kuchangia hapa na katika bajeti iliyopita mwaka jana nilizungumza kwamba Serikali inaweza ikawapa uraia pacha wale watanzania wanaokaa nje ya nchi, lakini ikawawekea condition ya kutokugombea nafasi za uongozi na hii itasaidia sana kuwawekea ile limit ya kuingia Serikalini.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukiacha kizazi cha Watanzania kukaa nje ya nchi bila kuwapa uraia pacha naona kama tunapoteza kizazi chetu ambacho kinakaa ughaibuni. Ukienda kwenye baadhi ya nchi unakuta kuna Watanzania kule wameoa wana watoto wana wajukuu yaani wanafamilia, yaani wana kizazi ambacho unakuta wanakwambia kwamba kizazi hiki asili yake ni Tanzania, wengi wao unakuta wamepoteza ule uraia wa Tanzania kwa sababu nchi yetu …

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpa mzungumzaji taarifa kwamba Serikali tayari inajipanga kutoa hadhi maalum na kupitia hadhi hii maalum Watanzania diaspora wataweza kupata haki zote kasoro tu kushiriki kwenye masuala ya kiasiasa pamoja na kufanya kazi kwenye vyombo vya ulinzi na usalama, ahsante.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbogo, Taarifa hiyo.

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana nafikiri kwa sababu Mheshimiwa Waziri atakuja ku-wind up atalielezea vizuri suala ambalo Mheshimiwa Neema…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa kengele ya pili, ahsante.

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Spika naunga mkono hoja Wizara ya Mambo ya Nje. (Makofi)