Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi kuchangia Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Balozi Mulamula nafahamu sio mwanasiasa ni mtendaji nakumbuka bajeti ya mwaka jana alizungumzia atatekeleza suala la uraia pacha na kuileta kwenye bajeti hii, lakini hata hajazungumzia na wala hajaingiza kwenye bajeti yake. Kwa hiyo nataka tu kumkumbusha aendelee kuwa mtendaji asitufuate sisi wanasiasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la viwanja, kiwanja cha Maputo kiwanja namba 157/1 wewe mwenyewe Naibu Spika ukiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje unafahamu ni kiwanja kipo zaidi ya miaka 40 enzi zile la Samora Machel na Julius Nyerere walipeana mpaka leo kiwanja kile hakijaendelezwa, hii imekuwa ni aibu kubwa sana kwa Taifa letu la Tanzania juu ya Balozi zinakuwa na viwanja vinakuwa vibovu popo wanaota mle kwenye majumba mabovu hii inajumuisha na nyumba kumi katika viwanja vitatu ambavyo vipo Zambia.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mama Mulamula, Mheshimiwa kiongozi Waziri ukienda Zambia viwanja vyetu vipo prime area kabisa ambayo sisi kama Taifa tulikuwa tuna uwezo wa kuvijenga viwanja vile, mimi nina uhakika Msechu yule wa National Housing Cooperation alikuwa na uwezo mkamwambia akajenga pale na akijenga pale, Mheshimiwa Waziri ana uwezo wa kusaidia corridor ya Kusini yote tukaweza zile fedha ambazo zitapatikana pale zikaweza kusaidia Balozi zetu za Kusini mwa Afrika, lakini nashangaa majengo yameoza, majengo ni mabovu mpaka wanafikiria namna ya kutunyang’anya. Hii ni aibu sana kwa Taifa kama la Tanzania lenye uchumi ambao una uwezo wa kujenga balozi zile. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na Balozi hizo wewe ni shahidi tunazo Balozi nyingi tumeshtakiwa majengo yanakuwa sio... Ufaransa kuna kipindi tulikuwa na jengo sio zuri sina uhakika kama mliendelea nalo na kulitengeneza.

Sasa Mheshimiwa nimesema wewe ni mtendaji sio mwanasiasa jitahidi kusimamie ile heshima yako uliyonayo ya kuisaidia Tanzania ikapata heshima ambayo tumedharaulika kwa muda mingi. Kiwanja kinakaa miaka 40 umri wa mtu anazaliwa anaoa anazeeka bado hatujaweza kukisaidia hicho kiwanja Mheshimiwa Spika naomba uingilie hilo, Naibu Spika naona na wewe kama kiongozi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukienda pale Abuja kuna kiwanja walitupa toka mwaka 1995 hadi leo wenzetu na kibaya zaidi kwa sababu mabalozi mnapopewa viwanja mnakuwa mpo wengi, kwa hiyo inaenda na lami inaenda vizuri, ikija kwenye Tanzania pana msitu unaenda tena sehemu nyingine Indonesia wananchi wamejenga Watanzani hatujajenga hii haiwezekani na wala haikubaliki…

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, muda wangu..

NAIBU SPIKA: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimpe taarifa mzungumzaji amekuwa anarudia maneno yake kwamba Mheshimiwa Waziri asiwe kama sisi wanasiasa. Sasa statement yake anatuchukulia wanasiasa wote hatuna credibility, kwani ni statement mbaya ya hovyo nataka nimwambie wana Siasa si kama wanavyojichukulia wenyewe, wengine ni wanasiasa tuna professionals zetu na tuna credibility, ahsante sana. (Makofi)

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee, naona ndugu yangu alikuwa ana hamu ya kuchangia. Sipokei...

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Sophia, ngoja basi.

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, sipokei...

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Sophia ngoja nikuite ndio nikwambie. Mheshimiwa Sophia, umeipokea taarifa?

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, sipokei naomba niendelee, naomba tuendele na suala la watumishi waliopo mabalozini najua kuna sheria ya utumishi unapompa mtu kazi akufanyie ni lazima uhakikishe stahiki zake zinakuwepo. Balozini kuna shida sana ya madai ya muda mrefu, kuna wafanyakazi wanadai unapowaongezea vyeo hawaendani sawa sawa na kipato wanachokipata, kuna madai ya nyuma ya safari na vitu kama hivyo tunaomba muwafanyie watu hawa stahiki zao ili waweze kufanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la diplomasia ya uchumi, tunashukuru Rais sasa hivi amerudi tena kwenye kuwasiliana na nchi mbalimbali tulikuwa tumepumzika kwa muda wa miaka kama sita, sasa ameamua kufungua upya. Ameenda kwenye Royal Tour na kweli tumeanza kuona mambo yakiendelea na wewe mwenyewe Waziri umesema kuna wafanyabiashara kama 100 kutoka Misri walikuja, na sisi hiyo tunaifurahia lakini pia Rais amefanya hiyo Royal Tour bado kuna shida kwenye mambo ya utalii ninajua kwamba mambo ya nje ya utalii vinaendana sambamba na hasa kwenye mambo ya hoteli. Kwa sababu utapata wageni sisi bado tupo chini sana kwenye industry ya kusaidia wageni tunaomba sasa wizara yako na Wizara ya Utalii kwa pamoja tusaidiane kusaidia wafanyabiashara wa kukaribisha hao watu ambao wanakuja kwa wingi tusipofanya vizuri hatutaweza kuingiza fedha na nguvu kubwa iliyofanyika tayari itakuwa imekwisha kupotea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Mabalozi mfanye kazi yenu ya kuhakikisha mnapochukua baadhi ya wafanyabiashara hapa na kuwapeleka nje wakaone wenzao wanafanya biashara vipi hasa za hoteli kwa sababu tunahaja na tunakaribia kupokea wageni wengi sana na bado industry yetu ya hoteli haijawa nzuri, watu wameendelea kuwa wavivu, watu hawafanyikazi kwa kujituma. Tayari wageni wanakuja ukipata wageni 100 na wewe unaanda chai saa nne badala ya saa mbili iwe tayari, tayari unakosa wateja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee kwenye suala la hiyo hiyo diplomasia ya uchumi; umesema kuna mtandao wa jb.com kule China ambao unaangaliwa na watu takribani milioni mia saba umesema, hawa ni watu wengi sana, lakini bado sisi pamoja na corona, lakini bado Tanzania kule Guangzhou ambao ndiyo mji wa kibiashara tulikuwa hatuna Balozi ndogo pale ni mpaka waende kwenye Balozi kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mji ukishakuwa wakibiashara lazima ujiongeze wewe kama nchi, tunafahamu nji ya jirani zetu sitaki kuwataja, wao hadi kwenye mabasi ya wachina kuna matangazo yao sisi tunashindwa nini! Mimi nimesema hapa kuna mmoja amesema nisikuambie wewe mwanasiasa bado ninakwambia mtu ambaye ni mtendaji haongei lugha mbili, ninaomba usimamie hilo uhakikishe kwamba tunaweka nguvu mpya ya kibiashara Guangzhou na tunapeleka matangazao mengi Guangzhou, tuhakikishe tunafanya biashara ya Guangzhou ili tuweze kukuza diplomasia ya uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya ninaendelea kuomba, ninaomba mama yangu chapa kazi, usimamie yale unayoyaamini kama nilivyosema wanawake wakiamini jambo lao wanalifanyia kazi, ahsante. (Makofi)