Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia kwenye Wizara hii muhimu ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Naibu Spika, natamani niwe na neno zuri la kumwambia Mama yangu Balozi Mulamula, lakini labda nianze kwa kusema unahitaji kufanya usafi kwenye nyumba yako, unahitaji kusafisha Wizara ya Mambo ya Nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mama Rais Samia Suluhu Hassan amejipambunua kutangaza Sera ya Mambo ya Nje, amejipambanua kwa kutangaza diplomasia ya uchumi katika nchi yetu. Na kwa kufanya hivyo ameona tofauti na watangulizi wake ana uwezo mkubwa wa kutuletea maendeleo Watanzania kupitia mahusiano na mashirikiano mazuri na mataifa mbalimbali hapa duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu hiyo, vipo vikwazo vingi ambavyo wewe kama balozi mbobezi ni lazima uviondoe ili kuweza kuifanya dhamira ya Mama Samia Suluhu Hassan iweze kukamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania tulikwenda Dubai, Marekani, tumefanya Royal Tour, tumeita wawekezaji, lakini kwa mfano Mkataba wa Kimataifa wa Huduma na Biashara ambao tuliingia mwaka 1994 mkataba ule unaruhusu wawekezaji kutoka nje kwenye maeneo mawili tu; eneo la utalii na usafirishaji kwa maana ya eneo la utalii na eneo hoteli kuanzia ngazi ya nyota nne. Sasa jiulize nguvu tunayotumia kutangaza, lakini kwenye eneo hilo la huduma tumeridhia kwenye maeneo haya mawili tu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, narudia tena mama yangu unakazi kubwa sana ya kufanya alignment ya sheria zetu, ya kufanya alignment ya mikataba mbalimbali ili wawekezaji waweze kuja kama ambavyo Rais wetu anawaomba na kuwasisitiza waje kuwekeza kwenye nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwekezaji yeyote duniani niliwahi kusema hii kwenye Wizara ya Viwanda na Biashara na leo narudia kwenye Wizara hii ya Mambo ya Nje, mwekezaji yeyote ambaye anatumia pesa zake kuja kuwekeza ndani ya nchi ni lazima afanye kitu kinaitwa economic intelligence lazima afanye intelligence. Hivi tunavyozungumza tunakwenda kuwatangazia kule lakini wanajua Shinyanga kunapatikana dhabahu na almasi, wanajua Arusha Mererani kunapatikana Tanzanite wanajua rasilimali tulizonazo, lakini kitakacho wakwamisha ni sheria zetu, mikataba yetu, tamaduni zetu na namna ambavyo tunakosa msimamo kwenye mazingira ya kibiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikutolee mfano, mwaka 2019 tulipitisha sheria mbili humu ndani zinasema sisi Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tutakuwa na uwezo wa kuitisha mikataba ya wawekezaji na kuipitia mikataba ile na kama hiyo mikataba itaonekana kwamba haiwanufaishi Watanzania kutokana na rasilimali zao mikataba ile inaweza kufanyiwa marekebisho. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi kwa clause kama hiyo ni nani anaweka kuja kuweka hela yake hapa, yaani kuna vifungu vya namna hiyo kwamba mtu anaweza akaingia mkataba akijua tumeshasaini deal, tumeshafunga mkataba lakini kesho asubuhi anaibuka Rais mwingine tofauti na Rais ambaye alikuwa labda ana nia njema anasema huu mkataba namna ulivyopitishwa pitishwa huu lazima tuufanyie review, tunafanyia review mwisho wa siku mkataba unabadilika ni unstable business environment. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na kwa sababu hiyo ndiyo maana hata unaona Mheshimiwa Waziri hicho kifungu hakitekelezeki, kwani tumeomba mara ngapi ilete mkataba hapa hakitekelezeki kwa sababu yaani haiwezekani ku-review mikataba kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa nchini tuna kitu kinaitwa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, tena kwa bahati nzuri Mahakama hiyo ipo Arusha hapa hapa Tanzania. Mheshimiwa Waziri unaomba fedha bilioni nne kwa ajili ya ujenzi wa mahakama na bilioni 1.2 kwaajili ya uendeshaji wa mahakama. Hakuna mtanzania au taasisi ya Tanzania inayoruhusiwa kwenda kufungua kesi kwenye ile mahakama na mwaka 2019 ndiyo tulijitoa kwenye haki hiyo.

Sasa mama yangu Mheshimiwa Liberata Mulamula utusaidie hii foreign policy na hii economic diplomacy anayoitangaza Mheshimiwa Rais inatokana na msimamo mzuri msimamo ambao una tabirika wa kibiashara ndani ya nchi mpaka mtu aje kuwekeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wamesema vizuri ndugu zangu hapa kuhusu suala la uraia pacha, tumeenda kuwavutia wawekezaji na baina yao ni Watanzania wanaoishi nchi za nje, tunasema waje kuwekeza, lakini unasema kwasababu anakaa nje nchi hawezi kuja kuwekeza huku ndani na kumiliki ardhi kwa sababu ni foreigner. Sasa mmoja ametoa taarifa anasema kuna kitu kinaitwa hadhi maalum, ni nini hiki hadhi maalum ni kitu gani? Kwa nini msiseme tunaposema hadhi maalum tunaamanisha itakuwa moja na mimi nilitegemea hivyo na ndiyo maana sikuhoji Mheshimiwa Rais aliposema kwamba watapewa hadhi maalum kwa sababu nilijua Mheshimiwa Waziri ukija kusoma hotuba yako utafafanua nini maana ya hadhi maalum na hilo ndilo swali la Watanzania wengi, na umesema vizuri wanachangia kwenye Pato la Taifa lakini ninani atakayekubali kwenda kuwekeza kwenye nchi ambayo hana uhakika kama mali anayoenda kuwekeza pale ataendelea kuwa nayo vizazi na vizazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Hawa watu wanafanyakazi ngumu diaspora, mimi nakuomba unapokuja kuhitimisha hapa uje utuambie hiyo inayoitwa hadhi maalumu ni kitu gani hasa humo ndani kuna vitu vya namna gani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka huu mwanzoni Waziri wetu wa Mambo ya Nje alipeleka ripoti ya utekelezaji wa haki za binadamu ambayo ni nzuri sana, mimi nakubaliana nayo, tume-adopt mambo mengi sana na moja kati ya jambo ambalo tulili-adopt tumesema hivi naomba ni quote; “The State supports the part of recommendation which leads to take all necessary measures to combat discrimination and violence against women including domestic violence” halafu mkaenda kukiri mkasema; “The State notes that part of the recommendation of on the family violence are this concept is yet to be define in the state policies” yaani sera zetu za nchi hazitambui au hazija accommodate suala la unyanyasaji (domestic violence) kwenye ngazi ya familia tumekubaliana nalo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri wewe unaona kwenye vyombo vya habari, jana kuna mwanamke Mwanza ameuwawa, leo tunaona hapa wamechangia vizuri sana wenzangu kwenye bajeti zao, watu wanauwawa, wanawake wanauliwa kwenye familia zao. Shinyanga asilimia 56 ya watoto wa Shinyanga wanaolewa wakiwa wadogo wanapata mimba za utotoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hii ni UN Report imepelekwa na Mheshimiwa Waziri anahusika, ndiyo mwenye dhamana ya hii ripoti yetu, ndiyo maana namwambia anatakiwa kusafisha nyumba yake. We have a lot of International Agreement ambazo hatuja ratify. Zipo International Agreement ambazo hatuja domesticate, hii yote ndiyo msingi, ndiyo tija, ndiyo shibe ya hiyo foreign policy ambayo Mama Samia Suluhu Hassan anahangaika kutembea duniani mama wa watu anamiaka sijui sitini na ngapi kuhakikisha kwamba anavutia wawekezaji. Sheria zetu, mipango yetu, mikataba yetu kama haiwalindi wawekezaji ndani ya nchi tutazunguka sana na jambo hili litakuwa ni la muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimalizie fedha tunayoenda kuwekeza kwenye African Court Peoples and Human Rights kama nimei-quote vizuri ni fedha nyingi, tufungue, kuna wakati mwingine haya mambo mnayafunga watu wanadhania kwamba mna nia mbaya yaani yanaonesha tu kwamba kuna dhamira ovu kwenye kufunga watu wasiende na taasisi, ruhusuni watu waende kwenye hizi mahakama rudisha kile kifungu cha 38 ili article tuliyo withdraw 38(6) nafikiri, rudusheni twende kwenye mahakama hizo tufungue, sisi ndiyo host na by the way umeomba fedha kwaajili ya kuendeleza mahakama hii, kwa nini unakataza wanachi wa Tanzania wasiende kushtaki kwenye mahakama ile, naelewa mazingira ya kisiasa yalivyokuwa mwaka 2019 wakati tunajiondoa, lakini mmejinasibu wenyewe kwamba huko tumetoka. Sasa hivi tuna uhuru wa vyombo vya habari, sasa hivi tuna uhuru wa waandishi, sasa hivi tuna uhuru wa watu kusema na mambo kama hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ni hivyo na hiyo mahakama ndiyo kazi yake kwenda kusikiliza watu wanaonyanyaswa waandishi wa habari, kwenda kusikiliza watu wanaonyanyaswa kwaajili wameongea na freedom of assembly, fungueni watu waende nchi ifunguke kama mnavyosema lakini tukisema tuna advocate, tunatangaza Tanzania ifunguke kiuchumi ilihali tunajua kabisa hapa yaani tunasema nini tunajipiga ngwala wenyewe, Mheshimiwa Liberata safisha nyumba yako, usimkwamishe Mheshimiwa Rais hatutaki kurudi kwenye kukusanya shilingi 20,000 za machinga. Mama analeta matrilioni ya fedha barabara zinajengwa, analeta matrilioni ya fedha vituo vya afya vinajengwa, biashara ya kuchangisha watu masikini tuachane nayo, fedha kwa ajili ya nchi zinaoendelea huko nje zipo kibao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo nakushukuru sana. (Makofi/Kicheko)