Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikushukuru kwa nafasi na naomba nianze kwanza kwa kuipongeza Serikali lakini hasa kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji wake wa hotuba yake kwa umahiri mkubwa sana hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba nimpongeze kwa kazi kubwa anayoifanya yeye pamoja na wasaidizi wake, hakika nchi imetulia, nchi imeongeza marafiki, lakini diplomasia yetu inaendelea kukua kwa kuongeza marafiki. Kwa sababu Wizara yako ndio Wizara ya marafiki, ni kazi ngumu sana kutunza marafiki, lakini kwa kweli umewatunza, endelea kuwatunza kwa niaba yetu sisi kama Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile naomba kidogo nikupe pole na nikupe pole kwa sababu unafanya kazi kubwa ya kuleta taswira yetu nzuri nje au duniani huko, lakini bahati mbaya sana kazi yako ni ngumu kwa sababu sisi kama Wabunge hatujafanya kazi yetu ya kukusimamia kuhakikisha unapatiwa uwezo wa kufanya kazi zako kama Wizara. Hakika huu ni wajibu wetu na hakika ni sisi ndio wa kujilaumu kwa sababu tunapoanguka huko kwenye mataifa kwamba hatuiwezeshi Wizara ni kosa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana tulisema hapa kwamba sisi kama Bunge tunakutana, tunapitisha bajeti nani apewe nini, lakini tunaiacha kwenye eneo fulani ili mmoja aamue kwa discretion yake, hii haijakaa sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lazima Bunge linapofanya maamuzi lichukue nafasi yake ya kuisimamia na kuishauri Serikali tunapopitisha bajeti, maana yake hatuchezi mchezo wa kitoto hapa, tunafanya kazi serious kwa ajii ya Taifa. (Makofi)

Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba nikupe pole kwa sababu ni kazi ngumu lakini fanya kwa sababu wanasema kazi ngumu mpe Mnyamwezi, I am not sure kama wewe ni Mnyamwezi au laa, lakini nikupe hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa maana hiyo hiyo naomba sana liko jambo la utekelezaji wa miradi ya maendeleo nimekusikia Waziri, lakini tumesoma hapa hotuba ya Kamati, kwa miaka miwili mfululizo Wizara hii haijapewa hata senti tano ya maendeleo. Sasa hili pia ni tatizo letu sisi kama Bunge kwa sababu wanasema duniani nothing is constant, maana yake ni kwamba changes ni kila kitu kinabadilika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ningeomba basi na niishauri sana Serikali kwamba tunapopanga kama Bunge na wenyewe waione kwamba Wizara hii ni muhimu ndani na nje kwa sababu ndio inayotuletea marafiki, ndio inatuongezea uchumi, inaongeza imani kwa wawekezaji tuwape nafasi na nyenzo za kuweza kutekeleza mipango yao ya maendeleo. Kama hatutaki waendelee tuwaambie kaeni msituletee mipango ya maendeleo, lakini haiwezekani tunakaa, tunapanga, tunapitisha, tunaamua halafu nothing is going on. Haiwezekani hii, ningeomba sana wenzetu hasa wenzetu wa Wizara ya Fedha mtusikilize Wizara ya Mambo ya Nje ndio kioo chetu duniani. Hakikisheni mnaiwezesha, msiiache kwa sababu ni wataalam hawapendi kupiga kelele mkaona hapana tutaiacha tu kama ilivyo, hakikisheni mnaiwezesha Wizara ili iweze kufanya mambo yake ya mipango ya maendeleo, ni lazima sio choice. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba nichukue nafasi hii kuwaomba wenzetu wa Wizara kwamba tuendeleze diplomasia ya uchumi kwa sababu tunayo maeneo yetu mengi duniani. Mimi nilijaaliwa kuishi India kuanzia mwaka 1992 mpaka mwaka 2000 pale Delhi tulikuwa na kiwanja chetu tumepewa miaka ya 1960, lakini mpaka tunaondoka mwaka 2000 kiwanja kile hakijaguswa na bahati mbaya sana kilichukuliwa wakapewa Ubalozi mwingine, sisi tukaishia patupu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumetafutiwa eneo lingine dogo, tumejenga, simply kwa sababu hatukuona umuhimu wa kujiendeleza au hatukupata nafasi, Wizara haikutoa fedha kwa ajili ya kuendeleza viwanja hivi. Ningeomba sana kwa viwanja vya aina hii au kwa nafasi za aina hizi tusidharau kwa sababu juzi tumekwenda Addis Ababa pale viwanja vyetu viwili tumenyang’anywa, sio kwa sababu Wizara haitaki, hapana, lakini kwa sababu utaratibu uliotumika lakini na sisi tumepewa hatukuweza kuviendeleza, hatukuona umuhimu huo. Leo tumerudishiwa lakini ninaamini tukizembea watachukua wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ningeomba sana hii ni nafasi yetu ya kukuza mahusiano, lakini na kukuza uchumi kama Taifa. Ningeomba sana tukubaliane, tuwawezeshe wenzetu, lakini maana yake wenzangu wamesema hapa kwamba tuhakikishe basi tunawashirikisha na wenzetu wa ndani, yako mashirika kwa mfano mwenzetu amezungumza National Housing Corporation wanaweza wakafanya, lakini ziko benki zinaweza zikafanya, lengo letu asset hizi zinajengwa na sisi zinatusaidia sisi, lakini zinajenga Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo ningeomba niipongeze Serikali pamoja na jitihada kubwa, lakini bado iendelee kufanya jitihada kwa sababu hatuwezi tukaishi, hatuwezi tukakuza Wizara ya Mambo ya Nje bila ya kuwaendeleza vijana wetu. Lazima tuwaendeleze kwenye mafunzo kwa maana tuanze kwenye recruitment, tuwafunze, lakini tuwa-place ili kuwe na kitu kinaitwa continuity, bila hivyo Wizara hii itaumia, inazungumza inajipanga, inatumia nguvu nyingi, lakini haipati nyenzo za kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)