Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kuungana na viongozi wenzangu wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa majaliwa yake kwetu sote, kwa jinsi alivyotuvusha kwenye majanga kama vile corona, ukame, mafuriko na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kwa niaba ya wananchi wote wa Jimbo la Mbulu Mjini kutoa pongezi za nyingi sana kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wetu mpendwa kwanza kwa kutunukiwa tuzo na kwa jinsi anavyotuwakilisha na kudumisha mahusiano na mataifa mbalimbali na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya mwaka 2020 - 2025.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mbulu Mjini nachukua nafasi hii kuwapongeza sana Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango - Makamu wa Rais, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa – Waziri Mkuu, Baraza la Mawaziri na watendaji wote Serikalini.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nampongeza Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula Waziri wa Wizara hii, Mheshimiwa Balozi Mbaruok Nassor Mbaruok – Naibu Waziri wa Wizara, Mheshimiwa Balozi Edward Sokoine - Katibu Mkuu wa Wizara, Mheshimiwa Fatma Rajabu Naibu Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii kwa kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya Wizara yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nitoe mchango wangu kupitia hotuba ya Wizara hii; kwa kuwa suala la kutokujengwa na kuendelezwa limechukua muda mrefu tunaiomba Serikali itafute fedha za kujenga majengo ya ofisi za Balozi zetu na makazi ya watumishi hata kwa awamu, kwani Serikali inatumia gharama kubwa sana katika kupangisha majengo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iangalie uwezekano wa kuwepo kwa maafisa wachumi wabobezi katika Balozi zetu na kama wapo watumike ipasavyo kwa kutangaza diplomasia ya uchumi na matumizi sahihi ya blue print na kutafuta fursa za mazao mbalimbali na bidhaa za nchi yetu katika masoko mataifa ya nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nchi yetu ina changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa ajira hapa nchini Serikali kupitia Balozi zetu ifanye uhamasishaji mkubwa sana makampuni ya nje kufungua viwanda vingi hapa nchini kwa kuondoa vikwazo na kuweka mazingira rafiki ili vijana wengi wa Kitanzania wapate ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa hivi sasa kumekuwa na wimbi kubwa sana la kusafirisha mazao ya chakula kama vile mahindi, maharage na kadhalika kwenda nchi za Afrika Mashariki, kuna hatari kubwa sana ya Taifa letu kukumbwa na baa la njaa. Serikali itumie njia za kidplomasia kuzuia hali hii bila kuathiri mahusiano yetu na mataifa hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga hoja mkono kwa asilimia mia moja na naomba kuwaslisha.