Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Wabunge tupitishe hii bajeti kwa sababu mimi vitongoji vyangu 374 tayari nimeshavipeleka REA na Januari nazunguka navyo kama unavyo nitakutumia tu sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, baada ya kusema hayo naomba mchango wangu uwe wa picha kidogo usiwe wa jimbo tu. Ni kwamba wakati tulitengeneza plan yetu ya miaka mitano tukawa tunasema tutaishia 2025 ilikuwa hivi; GDP per capita yetu lengo letu lilikuwa kufikia dola 3,000 na kufikia hapo tulikuwa na mipango au tunayo mipango ya umeme jumla installed capacity kuwa megawatt 10,000 mpaka megawatt 15,000 na ndugu zangu Wabunge nawaomba niwaeleze ukitaka uchumi ukue kwa zaidi ya asilimia nane kwenda asilimia kumi, unahitaji umeme mwingi na wa bei nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bei ya sasa ya senti 11 kwa unit bado ni umeme wa bei ghali. Sasa tulivyosema kama tukishindwa kufikia megawatt 10,000 mpaka 15,000, wakati tukiwa GDP per capital ya Dola 1,500 yaani nusu yake, tunapaswa kuwa na umeme installed capacity ya megawatt 5,000. Ndiyo maana ukiangalia kwenye document za Serikali zimewekwa kwamba kufikia mwaka 2025 tunapaswa kuwa na megawatt 5,000. Kwa hiyo, niwakumbushe tu kuwa na megawatt hizo ni lazima tuwe na vyanzo vingi, tujadili kila vyanzo lakini tusing’ang’anie kimoja, viwili bado hatutafikisha megawatt 5,000. Lengo letu ni megawatt 5,000 ifikapo 2025. Kwa hiyo, bado ndiyo maana nasema tupitishe hii bajeti ili kusudi tufike huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa upande wa umeme na maendeleo lazima ujilinganishe na ushauri wangu kwa Wizara nimeshawapatia Vitongoji 374, lakini mimi kuangalia maendeleo ya upatikanaji wa umeme nchini sitahesabu Vitongoji wala Vijiji, nitachukua hesabu ambazo zinatumika Kimataifa. Sasa Kimataifa unachukua unit ambayo Wizara inapaswa kutuambia ni energy per capital, yaani tukitupia vyanzo vyetu vyote tukagawa na population ya Milioni 62, je kila mtu ana unit ngapi, hizo ndizo zinahitajika. Lakini nzuri zaidi Vitongoji nimewapa nitakachoenda kuangalia mimi je, watu wa Kitongoji ‘X’ ni wangapi wanatumia umeme, ndiyo kipimo muhimu sana. Kwa hiyo, kwenye ripoti ya Wizara ninaomba mtoe ripoti ya energy per capital halafu mtoe electricity energy consumption per capital. Ukichukua hivyo vipimo unakuta kwamba Kenya, IMF inasema mwaka 2002 GDP per capital ya Kenya itakuwa Dola 2,252 na ya kwetu ni Dola 1,260.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wenye GDP per capital ya dola 1,260 Tanzania, installed capacity yetu ambayo imeandikwa Kimataifa na hiyo huwezi ukaidanganya kwa sababu unavyonunua turbines duniani wanaweka kwenye database, kwa hiyo wanajua nchi fulani wana uwezo wa kuzalisha umeme kiasi fulani. Kwa hiyo, installed capacity yetu ambayo iko reported Internationally ni megawatt 1,605.86. GDP per capital ya Kenya ambayo ni 2,252 wanazo megawatt 2,840, kwa hiyo lazima tushindane na Kenya kwa sababu alivyokuwa anaeleza Waziri transmission lines tulizozijenga za 400KV kupita Namanga na 400KV kwenda Zambia nia kubwa ni kununua umeme na kuuza umeme ndiyo uchumi wa kisasa duniani kote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ili tuweze kuwa na umeme mwingi tuendelee na hii miradi, energy mix yetu Tanzania ambayo ipo kwenye vitabu vyetu tumesema tutazalisha umeme kutokana na natural gas ya kwanza, pili itakuwa hydro, tatu itakuwa ni coal na nne itakuwa ni renewable energies. Sasa renewable energies zipo zaidi ya 11 lakini wengi wanajua solar na wind, lakini zipo 11 hiyo nayo kuna siku nyingine tutajaribu kuijadili. Lakini ukilinganisha na Kenya sasa, maana yake Kenya waliwahi kutuomba tuwauzie megawatt 1,000 ya umeme walivyokuwa wanaona miradi yetu inaenda kasi lakini sasa unaona wanatuzidi. Kwa hiyo sidhani kwamba wanategemea sisi tuwauzie umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, angalia Kenya wanavyofanya vizuri, kwenye geothermal wanazo megawatt 863, ndiyo wanaongoza Afrika kwa kuwa na megawatt 863, halafu Waheshimiwa Wabunge mmesikiliza michango humu matatizo ya ku-develop geothermal siyo kwamba yako Wizara ya Nishati havihusiani kabisa, completely outside the scope of the problems of geothermal energy development in the country, completely out. Kenye wind wanazo megawatt 437 linganisha na Tanzania, solar wana megawatt 173 sasa hizi nazitaja kwa sababu Tanzania tupo kwenye East African Power Pool, lazima tuuziane umeme. Halafu tuko kwenye SADC Power Pool kwa hiyo nadhani Mheshimiwa Waziri Wizara yako inavyotoa ripoti nzuri za Kitaifa lazima zionyeshe hali ya umeme ndani ya East Africa na ndani ya SADC kwa sababu sisi tunanunua umeme Uganda, sisi tunanunua umeme Zambia, sisi tunanunua umeme Kenya ndiyo maana tumejenga transmission lines tuzalishe umeme mwingi na sisi tuanze kuuza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nikiacha suala la umeme kwa ajili ya muda ninakuja kugusa kidogo kwenye mambo ya oil and gas. Muda usiponiruhusu nadhani nitaongea kwenye bajeti ile ya fedha kuhusu uchumi na gas. Kwenye oil and gas upande wa TPDC ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge ushauri wangu ni TPDC ambayo ilianzishwa mwaka 1969 iachwe na majukumu yake. Haya ya biashara ya mafuta kwa sababu waliopo pale TPDC ni Ma-geologist, Ma-geophysics, Seismologists, Geochemists wewe unawapeleka kwenye biashara ya mafuta haviendani na siyo eneo lao hilo! Kwa sababu TPDC bado kazi wanayoifanya hawajaifanya hata kwa asilimia 20. Wewe muulize TPDC inapaswa kutueleza Je, Tanzania kuna mafuta? ndiyo maswali tunauliza TPDC! Siyo kuuliza TPDC mafuta kwenye petrol stations za MOIL hapana! (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapaswa kuiuliza TPDC Je, Tanzania tunayo gas kiasi gani? Kwa mfano, sasa hivi Tanzania ni nchi ya 10, unajua wengi wanaongea tunayo gas nyingi, sisi ni wa 10 kwenye reserves kwa Afrika kwa dunia itakuwa kwenye mamia naongelea Afrika. Kwa hiyo ukiangalia Afrika ya kwanza Nigeria ina TCF 209, Algeria 159, Senegal 120, jirani yetu Msumbiji ana ripoti 100, lakini ambayo wanayo hawajaripoti wako kwenye 200. Ndiyo maana TPDC mimi sitaki iingie kwenye mambo ya kununua na kuuza mafuta kwa sababu hii gas 200 TCF za Msumbiji wamezipata Province ya Capo Delgado, ni kwenye Ruvuma basin. Sisi Ruvuma basin hatujaanza kufanya exploration, utaitoaje TPDC kwenye exploration na huko Kusini ndiyo tunayo gas nyingi kuacha hii tuliyonayo. Kwa hiyo, pendekezo langu mimi ni kwamba TPDC iwezeshwe na lakini siyo kununua na kuuza mafuta, iwezeshwe kufanya exploration. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kuna hii nafasi iliyopatikana vita ikipiganwa duniani, European Union asilimia 40 ya gas yake inanunua kutoka Russia, hizo ni 155 billion Cubic metric tons, 40 percent. European Union imezunguka nchi za Kiafrika kujaribu kununua gas lakini haijaja Tanzania kwa sababu sisi bado! Ndiyo maana TPDC waachwe kwenye core mission yao ya oil and gas exploration and development. Hata lile jina lenyewe jamani TPDC, Tanzania Petroleum Development Cooperation, haliitwi Tanzania Development Trade, unaona ile ‘T’, unaona tofauti hapo? Kwa hiyo tuwaache TPDC huko. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Mengine nitaongea siku nyingine. (Makofi)