Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

Hon. Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia Wizara hii ya Nishati. Nianze na mgogoro uliyopo kule Songwe, Mheshimiwa Waziri naomba anisikilize vizuri. Ni kweli Waziri ni mgeni katika Wizara hii lakini Maafisa wa Serikali wako pale na hasa TPDC. TPDC wametugonganisha kule Songwe, wametoa eneo moja linaitwa South Tanzania kule Kijiji cha Maleza, Jimbo la Songwe, kwamba wanakwenda kutafiti mafuta na gesi. Pale ukifika hata Mheshimiwa Kalemani wakati ule alishafika, wakaona ule uwanja na wakaanza kuona viashiria vya gesi na mafuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo watu wa kutafiti helium nao wakaenda, wakakuta kuna dalili hizo. Kwa hiyo wakawa wamepata certificate ya kwenda kufanya utafiti kwa ajili ya helium Wizara ya Madini, lakini vilevile TPDC wakatoa tena certificate ya wale wa heritage Tanzania wakafanye utafiti wa mafuta na gesi kwenye kitalu hichocho, kinaitwa South Tanzania. Sasa tunajiuliza Serikali ni moja hiyohiyo kwa nini mambo hayo yanatokea na hivi ninavyosema wananchi pale wanasubiri walishafidiwa mashamba, mahindi, kila kitu. Sasa naomba Mheshimiwa Waziri alichukue hili akaongee na watu wa TPDC waweze kuona jambo hili linakwendaje kwa sababu tunazo rasilimali tayari kule Ziwa Rukwa na mafuta yapo, kumbe gesi ipo, helium ipo, lakini ni just utafiti tu, mambo yamegongana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu Miradi ya REA kwenye Jimbo la Songwe. Miradi ya REA Jimbo la Songwe nashukuru Mungu kwa asilimia 30 bado kidogo vijiji vyote kuweza kutimia angalau asilimia 70 tayari, lakini hivi Vijiji vya Ngwara, Itiziro, Itindi, Maleza, Namkukwe, Manda, Isanzu, Muheza, Mpona, Ilea, Iyovyo na Kijiji cha Somi, vijiji 13 bado umeme, lakini tayari Mkandarasi ameshapatikana, ameshamwaga na nguzo, amechimba mashimo halafu akakimbia akaondoka, toka mwaka jana mwezi Septemba, mpaka hivi ninavyoongea Mkandarasi haonekani. Juzi nilikuwa Jimboni, nimetembelea Vijiji hivyo Mkandarasi haonekani kabisa, sasa sijajua Mkandarasi amepotelea wapi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna vijana ambao walikuwa wamechimba mashimo, wanadai fedha mpaka sasa hivi, wanamkimbilia Mbunge, Mbunge Serikali imetudhulumu, unajua wale kule hawajui masuala ya ukandarasi, hawajui masuala ya tender, sijui private company, no, wao wanachoangalia kwamba tunachimba shimo ili umeme uje, ni Serikali ndiyo imeleta umeme, ndivyo ilivyo. Kwa hiyo Mbunge akienda kufanya ziara pale, kwenye mkutano wa hadhara nimekutana na maswali sana Mheshimiwa Waziri, kwamba hawajalipwa fedha walizofanya kazi kwa ajili ya yale mashimo. Kwa hiyo naomba Mkandarasi aliyeshika tender kwenye Mkoa wa Songwe atafutwe haraka popote alipo akamalizie kazi kule ili umeme uweze kufika maeneo yale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa leo nilikuwa na hayo tu kwenye Wizara hii, otherwise fine Waziri anafanya vizuri, hongera sana. Ahsante sana. (Makofi)