Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kiongozi wangu kwa kunipa nafasi na kwa kweli kimsingi kabisa mimi niungane na Wabunge wenzangu kuendelea kuipongeza na kuiunga mkono Serikali yetu. Mimi kwa leo nina mada kama tatu chache kwa kifupi kwa ajili ya kuishauri Serikali yangu Serikali ya Chama changu iliyoko madarakani, kuwashauri Mawaziri wake pamoja na Watendaji wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwanza utafiti wa kidunia unaonesha kwamba Global Oil and Gas Companies ni state owned enterprise ambazo zinaendeshwa na Serikali husika duniani kote. Ili Taifa lolote liweze kufanikiwa katika exploration, exploitation kwenye mambo ya refinery, uuzaji na usambazaji wa oil and gas Taifa lolote duniani Waheshimiwa Wabunge na Mheshimiwa Mwenyekiti lazima lifanye uwekezaji wa kutosha katika taasisi zake za nchi kwanza, kwa sababu za kiusalama za nchi, lakini pili; kwa sababu za kibiashara za kupunguza makali ya maisha katika nchi yoyote ambayo imebarikiwa kuwa na resources ya mafuta na gesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia baadhi ya michango ya Wabunge humu na kidogo nimekuwa frustrated a little bit, katika dunia ya sasa hivi Waheshimiwa Wabunge itakuwa ni hatari kubwa sana, tukija hapa Bungeni tukatoa ushauri wa kui-discourage TPDC katika uwekezaji wa mafuta na gesi tutakuwa tunafanya kosa kubwa sana katika Taifa hili. Mataifa makubwa duniani yanayozalisha gesi na mafuta nenda nchi kama za Saudi Arabia angalia akina Saudi Aramco yale makampuni, nenda Venezuela, nenda Kuwait wameyawezesha mashirika yao ya ndani ya nchi kistratejia yameweza kuwa na mchango mkubwa wa kufanya biashara kubwa duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kwa Serikali, Kaka yangu Mheshimiwa January ninakuomba mimi sihitaji kusema sifa zako, uwezo wako wa kiutendaji brother hakuna mtu ana mashaka nao, uzalendo wako kwa nchi yetu Brother January na Naibu wako hakuna mtu ana mashaka nao, good enough umepewa timu ya Katibu Mkuu mchapakazi sana, Kaka yangu Mramba na mimi sifa moja January ambayo kwa kweli inakupa uziada, wewe ni humble sana Brother utasemwa utatukanwa mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Brother umepewa spirit ya ku-hold na kuvumilia mambo, keep that spirit lengo letu ni kumsaidia Rais na Serikali ya Chama chake kilichoko madarakani kufanya transformation. Hoja yangu ya msingi ninaomba Mheshimiwa January tengeneza mikakati, tunahitaji kuiona TPDC ya ushindani ndani ya miaka 10 tuweze kuwa na Shirika lenye uwezo wa ku-compete na akina Saudi Aramco tuweze kujenga heshima ya Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ninaloishauri Serikali yangu ndugu zangu tusitake kuishauri Serikali kuja kuangamia, wote tunajua gharama ya kupanda kwa mafuta duniani kumeathiri vitu vingi, leo tunazungumza hapa mimi January nakuambia hili usingekuja nalo kwenye mkakati, I swear mbele za Mungu wangu nilikuwa nakwenda kukamata Shilingi lakini brother mimi nasema kwamba mimi nimenyanyua salute kwako umefanya jambo la diversification ya umeme na umetuambia unakwenda kuongeza kilomita mbili kila kijiji hivi jamani kwa strategy hizo atajitokeza Mbunge hapa aseme mama Samia hafanyi kazi? Au akisimama mtu kusifia mnasema eti wengine wanatumika? Unatumikaje kwa mambo mazito kama haya Rais anayoyafanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaambie wala msidanganywe Rais asidanganywe Wabunge wote humu ndani wanampenda Rais na wanamuunga mkono, watu wasiende kutaka kuwachongea Wabunge na Rais waonekane kwamba kuna baadhi ya watu wazuri baadhi ya watu wabaya, Mama Samia kwa kazi anazozifanya wewe Mbunge kama huungi mkono wewe ni kichaa. Leo tunazungumza hapa hii bajeti Mheshimiwa January umeleta hapa kwa diversification unakwenda kuifanya ya umeme ina maana Mama ameweka bajeti amekwenda kui-triple mara mbili, vijiji tunaongezwa kila kijiji kilomita mbili nani kama mama Samia jamani! Kweli na hili nikisema mje mseme kwamba Kingu anazungumza ili ajipendekeze hivi, mimi ni kijana msomi jambo la kwanza, halafu siyo msomi mimi hapa kichwani niko vizuri. Nikija kujenga hoja hapa ninajenga hoja kwa sababu walipa kodi waliotutuma wamepata matumaini makubwa ya kazi zinazofanywa na Serikali Awamu ya Sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu January kaka yangu ninawashauri ni kweli bei imepanda msije mkajidanganya hapa tukataka sifa hapa ooh! Wakandarasi wanaiba bei zimepanda msiwaumize Wakandarasi bei zimepanda za vitu fanyeni utafiti tumieni wataalam wakaangalie quoted BOQ zilikuwa ngapi? Waende kwenye market ya sasa hivi, waangalie bei inasoma ngapi, nendeni mkawaongeze wakandarasi pesa miradi ya mama iishe miradi ya Mama iishe, lengo letu ni kuhakikisha ya kwamba kwa hali Mama anavyoupiga mwingi coming 2025 Rais ajichukulie kura kutoka kwa Wabunge hawa ambao ndiyo wasemaji na wawakilishi wake huko kwenye Majimbo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho tulizungumza hapa Bunge lililopita and I was one of the MPs ambao tulishauri ile kampuni mliipa kazi ya kuweka vinasaba kwenye mafuta we spoke of this, ilikuwa ina-charge Shilingi 14 kwa lita watu wakapiga kelele hapa mbona tunaibiwa, Rais ameingia madarakani Mama Samia ametoa maelekezo tangazeni tender.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tender imetengazwa huyo ambaye yupo sasa SISPA ameomba na makampuni mengine, mchakato umeenda, kampuni imeshinda inatuambia itatuwekea vinasaba kwa shilingi 5.8 kwa lita hao SIPSA nasikia sijui wametenda shilingi nane, wameshinda kampuni lowest mmefuta tender hivi mnafanya kwa maslahi ya nchi au kwa maslahi ya nani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunapozungumza hapa projection zinaonesha Serikali inapokea loss ya shilingi bilioni 4.5 kila mwezi, hivi jamani hatuionei huruma hii nchi, hizi bilioni 4.5 kila mwezi tunazopata loss, sitaki kusema mengi. Ushauri wangu kwa Serikali…

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Salome Makamba taarifa.

T A A R I F A

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpa taarifa mzungumzaji Mheshimiwa Elibariki Kingu hasa kwenye ile jambo analolizungumzia la ufutwaji wa tender. Sheria ya Manunuzi ambayo tulitunga wenyewe ndani ya Bunge hili kifungu cha 19(1), (2) na (3) kinataka utaratibu wa kufuta tender Bodi ya Zabuni waende kuomba PPPRA na baada ya kuomba uchunguzi ufanyike na waitwe wale walioathirika baada ya kufuta tender ile lazima waitwe ili waweze kutoa concern zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kama utaratibu wa ufutwaji wa hiyo tender ambayo wote humu ndani tulikubaliana kwamba wakapewe ile kampuni nyingine badala ya hii inayotia Taifa hasara, kama utaratibu haukufuatwa Mheshimiwa Waziri huu ni uendelezwaji wa uvunjwaji wa Sheria ya Manunuzi ambao unafanywa na Serikali katika idara mbalimbali za nchi hii naomba nikupe hiyo taarifa. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kingu unapokea taarifa.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa unyenyekevu mkubwa taarifa ninaipokea kwa unyenyekevu mkubwa sana. (Makofi)

MWENYEKITI: Haya endelea.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndiyo maana haya mambo tunasema, unajua hili taifa tunalipenda wote, ikiwa Rais aliona kuna mahali kuna shida, mama yetu akaagiza haya yafanyike, hayo yaliyofanyika ya kufuta tender na ninakwambia hapa leo nina kwa mambo haya I have statistics zinaonesha wale watu wa TBS wanapoteza shilingi 11,000,000 kila siku; shilingi milioni mita tatu karibia na sabini kwa mwezi ukiangalia hata trend nzima kwenye nchi ndio nimekuja kufanya compilation nimepata fedha zinazopotea 4.5 billion kila mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge mpo tayari bilioni 4.5 zipotee fedha ambazo zinaweza kwenda kutumika kusaidia watu wengine? Serikali chonde chode msimtie Rais wetu doa, msimtie narudia tena nazungumza nikiwa na macho nimeyakaza bila kumwogopa mtu msimtie Rais aliyepo madarakani doa, fuateni taratibu na sheria za nchi mama huyu kazi anazozifanya kwa Taifa hatutaki 2024 kwenda 2025 Rais wetu tunapomnadi tunataka ni kutoboa na kuteleza kwa maslahi ya Taifa…

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwambe taarifa.

T A A R I F A

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimuongezee taarifa Mheshimiwa Kingu kwamba Kampuni hii anayoitaja ya SISPA ndio pia inayoendesha sasa uchapaji wa zile stempu za kieletroniki za ETS. Kwa hiyo malalamiko haya ni mapata kwenye uwanda wa biashara zinazofanywa na SISPA wakati nchi nyingine zilimkataa na ushahidi upo hata mimi ukiniambia nitenge ushahidi kwako nitakuletea. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kingu, unapokea taarifa?

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa unyenyekevu mkubwa ninapokea taarifa…

MWENYEKITI: ...na muda wako sasa umekwisha.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutoka kwa Mbunge makini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo ninaunga mkono hoja Mheshimiwa January na Naibu wako fanyeni kazi mumsaidie Mama, Bunge na Watanzania tupo na ninyi mpaka kieleweke. (Makofi)