Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona na kunipa fursa hii, nitazungumza machache na nitaomba nisitoe pongezi kwanza nimalize kwanza kwa sababu muda wangu ni mfupi na mimi nina mambo mengi ya kusema, lakini nitakuwa nakosa fadhila nisipoanza kumshukuru Mheshimiwa Rais wetu ambaye wote tunasema tunampenda sana, lakini sisi Wanavunjo tunampenda zaidi kwasababu tumeona miradi mingi imekuja pamoja na kwamba mradi wa ujazilizi (densification) ya umeme ulikuja kuzinduliwa pale kwetu kwenye Kijiji cha Nganjoni na ninashukuru sana ni jambo la kumshukuru Mungu sana kwa sababu kwa muda mrefu kule Vunjo tulikuwa hatujaona miradi kama hii chini ya Awamu ya Sita namshukuru sana pia Waziri anayehusika Mheshimiwa Makamba na uongozi mzima wa Wizara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme pamoja na kwamba tulifaidika na tulikuwa na bahati ya kuzinduliwa mradi wa densification, lakini ule mradi haukuendelezwa, naona umeanzia pale kwenye Kijiji cha Nganjoni kwenye Jimbo letu, lakini naona haujaendelezwa sana, lakini pia kuna tatizo kubwa sana na ambalo tumeambiwa na tunamshukuru Waziri ametuletea watendaji wetu kwenye mabanda tukazungumza nao wakasema kwamba sasa fedha zimepatikana za kuweza kuwaunganisha wananchi wetu ambao tayari wameshalipia kufungiwa umeme kwa miaka zaidi ya mitatu, lakini hawajafungiwa wananchi zaidi ya 2,500 kwa Wilaya yetu ya Moshi Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tumeambiwa kwamba fedha inapatikana na mpango upo sasa na vifaa vipo, kwa hiyo, wataanza kufanya hiyo kazi na ninaamini kwamba wakati huo hawadanganyi na ninaamini kwamba Waziri tuliye naye ni makini, ataweza sasa kutuhakikishia kwamba hii kazi itafanyika kwa sababu kusema kweli ni kazi ambayo inaendana na kipaumbele chake cha kwanza japokuwa ninaamini kwamba vipaumbele hivi viliorodheshwa vya kwanza mpaka kumi na viwili sio kwa umuhimu wake kwamba vyote vitatekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipoanza kusoma hotuba ya Mheshimiwa Waziri na naomba nieleze pale alipoishia Mheshimiwa Vita Kawawa jana, nilijiuliza maswali machache; swali la kwanza kwamba je, Wizara inaweza ikatuambia mahitaji au makisio ya mahitaji ya umeme hapa nchini katika kipindi cha miaka mitano kwa uhakika yakoje? Kwa sababu ukiangalie kwa miaka 60 tumekuwa na uzalishaji ambao haujazidi megawati 2,000; uzalishaji ulipo kutokana na kielelezo cha kwanza kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri ni megawati 1,694 na nimekuja kuangalia matumizi ya kiwango cha juu wanasema kiwango cha juu cha matumizi ni megawati 1,335 na miaka 60 ya uhuru. (Makofi)

Sasa ninapoangalia tukienda na uzalishaji huu ambao tunaambiwa nao unaongezeka kwa kasi tukiweka Kinyerezi Extension megawati 185 tunaweka Rusumo megawati nane, tunaweka Nyerere megawati 2115 tunakuwa tumeshaongeza megawati 2,700; ni karibu mara mbili ya matumizi yetu ya sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini bado kuna mingine, kuna hii ya Ruhudji, Kakono, Rumakali, Malagarasi na kuna Kikonge ukiongeza yote hiyo tunakuja kuwa tunaongeza katika haya matumizi yetu tumeshaongeza megawati 4,205 na ukiweka kwenye hii ambayo tunayo tunafikia megawati 5,899. Je, mahitaji haya tunajua tutayatumia kweli kwa kasi hiyo? Kwa sababu kama tunatumia megawati 1,300 sasa tunakuwa na megawati 5,800 makisio ya matumizi yako hapa huwezi kuongeza kukimbizana na ongezeko la uzalishaji au kupanua uzalishaji bila kuwa na uhakika kwamba utapata wanunuzi wa matumizi kwa sababu ni fedha tunaweka na hii fedha tunayoweka kwenye umeme kwa kasi sana tunataka umeme uwepo wa ziada, lakini sio kwa ziada sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tunatumia fedha za kukopa kwa kutengeneza miundombinu hii, kwa hiyo lazima twende na kasi ambayo inakubalika, kasi ambayo nayo pia itapunguza ukopaji, kasi ambayo itahimilika. Tukiweka tu for the sake tutakuwa tunajiingiza mahali pabaya, lakini tungeweza kuhakikisha kwamba tunajua vianzio na vianzio vile tunajua deploy quickly na vingine vinachukua muda sana hiyo ni moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili suala hili la subsidy na suala hili la kuhifadhi/kuweka strategic reserve ya mafuta. Mimi nafikiri hivi tuangalie options za hii kwa sababu unaweza ukaweka akiba kwenye fedha au ukaweka akiba kwenye bidhaa; ukiweka akiba kwenye bidhaa ya mafuta, bidhaa ya mafuta inabadilika badilika bei, kwa hiyo unaweza ukanunua mafuta leo ni dola 100 kwa bulk, lakini baada ya siku chache hizi zinazokuja miezi mitatu ikaja mafuta yakashuka bei yakawa dola 73 kwa bulk, utakuwa umeshapata hasara ya dola 25 kwa bulk.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ungeweza ukanunua option futures option, future options ni kwamba unailipia premium kidogo lakini yule m-supplier atakwambia endapo unahitaji mafuta kwa mwezi unaokuja wa Juni, mwezi unaokuja wa Julai, Septemba, utampa stagged delivers.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila staggered delivery inategemea ni muda gani unailipia premium yake na ile premium unayolipa ni option kwamba naweza nikanunua au nisinunue. Kama itakuwa bei imeshuka sitanunua kwa ile bei ambayo nimei-hedge kama ikipanda basi nitanunua kwa sababu najua kwamba nimekua nimei-hedge ile bei kwa bei ambayo ni ya leo na bei ya leo ndiyo hii sasa nimeshalipa subsidy na ile subsidy badala ya kuitumia kugawa ingetumika kununua futures options za kuletewa mafuta kwa bei ambayo tunaijua ya leo, hapo utakuwa ume-stabilize. Pia itapanda huna pressure ya kwamba bei itapanda halafu nitanunua kwa sababu umei-hedge na ile gharama ya ku-hedge ni very little ya ile volume ambayo tunaweka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naamini kwamba tukae chini wale watu ambao wanajua financing na hizi hedging na features tufanye kitu ambacho kinakubalika kitakaa forever na kila wakati TPDC ipate hiyo option ya formular inanua mafuta kwa bei ambazo zinajulikana leo lakini kwa ku-deliver in the feature kama ni six months. Kwa sababu kama wewe utanunua tu yaani hivi vitu haviendi tu kiholeholea utapata hasara, tutakuja kupata hasara tuhangaike bure. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni kwamba tunapozungumza suala zima la kuzalisha na mimi nakushukuru sana, kipaumbele alichokiweka pale cha uzalishaji na usambazaji. Wanasema hivi, asilimia 78.4 ya Watanzania wamefikiwa na gridi, lakini watu waliounganishwa kwenye gridi ni asilimia 37.7 tu! Wengine hawajaunganishwa na wengine wanaotumia tunasema umeme upo lakini watu wanaotumia solar na tunashukuru Serikali hii tukufu ambayo iliweza kushusha VAT kwenye solar panels, sasa watu asilimia 30 ya Watanzania wanatumia solar! Kwa hiyo, inakuwa about 66 percent ya Watanzania wanapata umeme lakini wengi nusu yao wanapata kwa solar lakini umeme wa solar hauwezi kufanya mambo fulani fulani ya viwanda na nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pamoja na hela tulizonazo nyingi hizi tujaribu kuona ni wapi tukimbizane napo ambako ni kusambaza umeme wa gridi ku-stabilize ili kile kiwango tulichonacho kiweze kutumika vizuri kisipotee na kila mtu aweze kupata umeme ule usambazwe ufike kwenye nyumba zetu na kwenye viwanda vidogo vidogo na kwenye maeneo yetu, shuleni na kwenye hospitali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikifanyika hivyo sasa tunaanza kuona tija ya hiki tunachozalisha na hicho ambacho kinapangwa kuzalishwa kwa kuongeza tusikimbizane tu tunafuta lakini tunataka ufafanuzi je, mnasema mta-export kama mta-export; je, mna bei za ku-export kweli ambazo mmeshazifungamanisha vizuri mkajua kwamba mtapata faida? Tusije tuka-subsidize kwa wenzetu umeme na sisi tumejenga kwa fedha ya kukopa hiyo ni moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwamba pengine kitu ambacho kingetakiwa pia tukiangalie ni suala zima la kujua mikakati gani hili suala la stabilization project kwamba je, itatekelezeka kwa muda gani? Kwa sababu fedha ambayo inahitajika sidhani kama imetengwa yote, walisema Bilioni 500 au Milioni 500, naona hata muda wa kuzungumza unaisha lakini ninaunga mkono hoja, naamini kwamba kweli kuna mambo mazuri yanafanyika kwenye Wizara na mimi nampongeza sana Mheshimiwa January kwa yote hayo anayofanya, waendelee kufanya na waendelee kutuletea vitu vizuri, summaries ambazo zimekaa hivi zinasaidia. Ahsante sana. (Makofi)