Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

Hon. Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa dakika tano ulizonipa, ahsante sana. Nami niungane na wenzangu kuipongeza Wizara na Serikali kwa ujumla. Kwa dakika tano hizi naomba nizungumze jambo moja suala la REA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikiliza michango ya Wabunge wenzangu humu ndani wamezungumza kwa hisia sana na wamezungumza kwa hisia kwa namna mradi wa REA unavyotekelezwa kwenye Majimbo yao. Pamoja na hisia hizo baadhi ya Wabunge wenzangu atakwambia vijiji vilivyobaki katika Jimbo lake 10, 11, 12.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa masikitiko makubwa jimbo langu linavijiji vikubwa vipo 117, kati ya vijiji hivyo vijiji vilivyopata umeme ni vijiji 34 na kwa bahati mbaya kati ya vijiji hivyo 34 vijiji Tisa zimesimikwa nguzo tu lakini tunasema vimepata nini umeme, vijiji 86 vyote havina umeme, Kata 15 hazina umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemuomba sana Roho Mtakatifu anishukie hapa nizungumze kwenye kona zile za Mheshimiwa Spika. Kwa sababu wenzangu wamezungumza hapa kwa hisia kali sana ni vijiji 10,15, 20, mimi vijiji 86 ongeza Tisa ni vijiji vingapi havina umeme? Kwa hiyo, kwa masikitiko makubwa sana, nashukuru sana Mheshimiwa Waziri nakuheshimu sana na bahati nzuri nilikuja kukuona umenipa ushirikiano mzuri, ukanikutanisha na Mkurugenzi REA naye alinipa ushirikiano mzuri akanikutanisha na Wakurugenzi wake, Wasaidizi wake na bahati nzuri akamuita na Mkandarasi. Kwahiyo, niombe yale tuliyokubaliana yale tuliyozungumza na moja ulilolisema ni kuja Mbinga kuangalia hali ya utekelezaji wa huu mradi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua ujio wako utatoa push sasa tunasema vijiji 23, vijiji 9 zimesimikwa nguzo tu, nguzo imesimikwa hivyo vijiji vingine mwenzangu alisema hapa jana kwamba utekelezaji wa huu mradi ni 0.5, maana yake ni kama wameenda ku-survey tu, yaani wamefanya survey tu na pengine wamelaza nguzo. Kwa hiyo, kwa ujumla mradi huu Jimbo la Mbinga na nilimwambia waziri sehemu itakayokuonesha wewe umeshindwa kutekeleza mradi huu kwa asilimia 100 ni Mbinga na kama si Mbinga basi Mkoa wa Ruvuma kwa sababu hata Tunduru kuna vijiji 86 havijaingiziwa umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe sana Waziri atakapofanya majumuisho hapa atueleze namna ya kasi itakavyokwenda katika Jimbo la Mbinga Vijijini ili ifikapo Desemba kama walivyoahidi nasi vijiji vyetu vyote viingie kwenye umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine napata faraja kidogo wanasema kawia ufike, nimeona kwenye hiki kipeperushi kwamba tunaenda kusambaza umeme sasa kwenye vitongoji hasa kwa vile mimi vijiji vyangu 86 havipo kwenye mradi huu vimechelewa kuingia kwenye mradi wa umeme; 86 sasa tunaenda kwenye vitongoji ninauhakika tutaanzia huko na vitongoji kwamba sasa vitongoji vyote na vijiji vyote vitapata umeme ninauhakika huo najua hautaniangusha hapa kwasababu tumechelewa kusubiri umeme sasa tuna bahati sasa tunaaanza vitongoji na kwasababu sisi tulichelewa zaidi basi tutaanzia hapo ndiyo maana nimefarijika kusema kawia ufanye nini? ufike na kutangulia sio kufanya nini? kufika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliona niseme hilo tu kwa hizo dakika na nashukuru sana kwa kuniruhusu. Ahsante. (Makofi)