Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutujalia amani, upendo, afya, mshikamano na utashi wa kisiasa katika Taifa letu. Aidha, tunampongeza sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan - Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango - Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa usimamizi wao thabiti katika utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2022-2025.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawapongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Spika wetu, Mawaziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na watendaji wote Serikalini kwa kuitumikia vizuri sana nafasi zao kikamilifu hongereni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaiomba Serikali na Wizara waangalie upya wa kutafuta fedha zaidi katika kufanikisha mpango wa kupeleka umeme kwenye vijiji ambavyo bado hadi sasa line kubwa haijafika ili kurahisisha utekelezaji wa dhamira ya Serikali yetu na Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa malengo ya Serikali ya kupeleka umeme kila kijiji unasubiriwa na wananchi kwa hamu kubwa sana, na kwa kuwa bado kuna maeneo makubwa ambayo makandarasi tayari wamesimika nguzo zaidi ya miezi sita sasa, tunaiomba Serikali iwalipe makandarasi fedha zao kwa kazi ambayo tayari wamekamilisha ili waweze kuwasha umeme katika baadhi kwenye majimbo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mapendekezo ya hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati kiasi cha fedha zilizotengwa kusambaza umeme vijijini awamu ya tatu mzunguko wa pili ni kidogo sana kulingana na mahitaji halisi ya mradi huu wa shilingi bilioni 1.240. Hivyo basi ni muhimu Serikali iangalie mpango mbadala wa kutafuta fedha zaidi, na mradi huu ni muhimu sana ukaanza kwenye vijiji ambavyo line kubwa ilishapita kwa zaidi ya miaka mitatu na maeneo yenye uzalishaji mkubwa kwa mfano taasisi za umma na binafsi, taasisi za dini, migodi, vijiwe vyenye biashara na maeneo ambayo yana uwezekano wa kuanzishwa viwanda vidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Mheshimiwa Waziri kupitia hotuba yake aweze kutoa kauli ya Serikali kuhusu matumizi sahihi ya unit kwa watumiaji wadogo hususan umeme wa matumizi majumbani. Kwani eneo hilo lina mkanganyiko kati ya TANESCO na TRA, na wananchi wa kipato cha chini vijijini kuona tofauti ya umeme wa matumizi na ule wa kibiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho siyo kwa umuhimu, tunaiomba Serikali itume utafiti kuzalisha umeme wa upepo ili kuongeza vyanzo vya umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.