Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

Hon. Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

MHE. NANCY H. NYALUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Wizara ya Nishati kwa kazi nzuri wanayoifanya na mikakati mizuri ambayo wameipanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza TANESCO kwa mfumo rahisi wa maombi ya huduma ya umeme kwa njia ya mtandao ambayo inamuwezesha mteja kupata huduma mbalimbali bila kufika katika ofisi za TANESCO. Natoa rai kwa Serikali kutoa elimu zaidi kwa wananchi ili wauelewe mfumo huu ili kupunguza usumbufu na mazingira yote ya rushwa na kurahisisha upatikanaji wa huduma ya kuingiza umeme kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaishukuru Serikali kwa hatua kubwa ya majadiliano kuhusu mradi wa LNG Lindi. Ni hatua gani majadiliano yamefikia mpaka sasa na lini mradi huu utaanza na kampuni zipi zinahusika na mradi huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri anipe maelezo kama kuna National Fuel Reserve; kama ipo ni kiasi gani? Katika changamoto tunazopitia za upatikanaji wa mafuta kama nchi ni lazma tuwe na Strategic Fuel Reserve. Serikali ianzishe Fuel Price Stabilization Fund ambapo kukitokea kuvurugika kwa bei ya mafuta duniani Serikali iweze kuingilia kati na kutumia hii fund kutuliza bei za ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na nawatakia utekelezaji mwema wa vipaumbele vya bajeti.