Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kuwapongeza kwa hotuba ya bajeti ambayo iko well detailed, aidha, nawapongeza kwa ubunifu wa kutuletea maonesho hapa kwenye viwanja vya Bunge. Ilitusaidia sana kupata uelewa sio tu wa masuala ya umeme lakini nishati kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ujumla utendaji wenu kuanzia TANESCO hadi REA ni wa kuvutia na shirikishi. Aidha, kwa niaba ya wananchi wa Mafinga, Mufindi na Mikoa yote ya Iringa na Njombe tunawapongeza na kuwashukuru ambavyo tumeshirikiana katika suala la Serikali kukubali kuendelea kununua nguzo za umeme hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu; ninatambua kwamba ni haki ya kila Mtanzania kufikishiwa umeme. Hata hivyo pamoja na kuwa umeme ni huduma, lakini pia ni biashara, kwa sababu hiyo nashauri baadhi ya maeneo kama Mafinga na Mufindi ambako kuna viwanda vingi tuanze kuelekeza nguvu huko ambako umeme ni biashara ili TANESCO ipate returns ambayo itaenda kugharamia umeme kule ambako wao ni huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri huu ni pamoja na kutufungia transfoma zenye KV kubwa na kuwapa TANESCO bajeti kubwa. Hili linaweza kufanyika kwa kuangalia tu mapato katika maeneo hayo kama Mufindi, mtabaini wazi kwamba TANESCO inapata mapato makubwa, kwa hiyo, hapa tunapopata mapato makubwa tuongezewe nguvu ili mapato yaongezeke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa muktadha huo nawasilisha maombi ya Mradi wa Ujazilizi kuwa na wigo mpana hasa katika vijiji vya Halmashauri ya Mafinga Mji ambayo administratively ni mji lakini una vijiji kumi na moja, ambapo Kijiji kama Matanana wananchi wana mashine za kuchana mbao lakini wamezifungia ndani kama ambavyo wananchi wa Kata ya Sao Hill ambapo kuna ujenzi wa shule ya sekondari chini ya mradi wa SEQUIP wamefungia ndani mashine zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali iko sawa katika Kijiji cha Ndolezi na pia Mitaa ya Luganga, Mtangani, Majengo mapya katika Kata ya Wambi. Hali hii pia iko katika Mtaa wa Lumwago ambao wanaishi vijana wengi wanaojenga kwa kasi sana, kama ambavyo hali hii ipo Ifingo, Miami na Kijiji cha Rungemba na Itimbo ambako kuna eneo kubwa la viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa sababu hiyo nashauri kwamba densification na bajeti ya TANESCO walau iongezeke kuendana na kasi ya ukuaji wa Mji wa Mafinga na hasa kuelekea katika maeneo ya uzalishaji kwa maana ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuwa nimeshatuma mchango wangu kwa maandishi, nimewiwa kushauri jambo kuhusu LUKU, je, hatuwezi kutumia mifumo ya kisasa kama tunavyofanya katika huduma za ving'amuzi ambapo ukinunua tu inaji-update yenyewe automatic? Nashauri tuje na mfumo huo.