Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

Hon. Saada Mansour Hussein

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, natumia nafasi hii kuipongeza Wizara ya Nishati chini ya ndugu yangu Mheshimiwa January Makamba kwa kazi kubwa anazozifanya kwa kuhakikisha Taifa letu linaendelea kupata umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu ni kuhusu Bwawa la Mwalimu Nyerere lililopo Rufiji, napongeza ujenzi kufikia asilimia zaidi ya 60. Bwawa hili ni muhimu sana kwa maendeleo na pia tunalitegemea kuboresha hali ya umeme hadi Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano mkoa wangu wa Kaskazini Unguja kuna uwekezaji mkubwa wa hoteli kubwa na ndogo ndogo, ujenzi wa hoteli hizi kwa kiwango kikubwa utakwenda kusaidia wananchi kwa kupata ajira na fursa za biashara. Aidha bwawa likikamilika uzalishaji ukianza hoteli zitapata umeme wa uhakika na wananchi wa Zanzibar watafaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Wizara ihakikishe fedha zinapatikana kwa miradi yote kutoka Hazina kwa wakati ili ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere usikwame na uende kwa muda. Ahsante.