Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

Hon. Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Nishati

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mungu kwa ajili ya Mheshimiwa Rais Mama Samia kwa kazi nzuri anayoifanya kwa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza Wizara nzima ya Nishati kwa kazi nzuri pamoja na changamoto zilizopo, lakini mmekuwa mnapambana nazo na zinaendelea kutatuliwa, hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe kuchangia kuhusiana na Jimbo la Temeke ukizingatia ni mji mkongwe na miundombinu ya umeme ni ya muda mrefu. Kwanza nguzo nyingi zimeoza hivyo kupelekea kuanguka kila mara na wananchi kukosa umeme, lakini pia miundombinu inayopita chini ya ardhi inasumbua muda mrefu, niiombe Wizara hii iangalie namna Temeke itakavyoweza kurudi kwenye hali ya kawaida kwani bado umeme wetu tunapata kutokea Ilala. Ni mkakati gani sasa Serikali itafanya kuhusu Temeke kwani ni jimbo lenye viwanda vingi, umeme hautoshi na tunakosa mapato ya ndani kwani kila tukitembelea viwandani umeme haupo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana mtuangalie upya kwani hali si nzuri, hata TANESCO mnakosa mapato kwani viwanda vingi hawalipi kulingana na utumiaji wa umeme kwani umeme ukipatikana kwa mfululizo nao watafanya kazi kwa muda mrefu na bill zitakuja na kuleta mapato ndani ya Shirika la TANESCO. Niiombe Wizara itushughulikie tupate umeme katikati ya Jiji la Dar es Salaam ambalo ni jiji la biashara, kukosa umeme haieleweki, mtuangalie. Ahsanteni sana.